Waziri Membe jiandae kukanusha

Waziri Membe jiandae kukanusha

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Nazungumza nawe Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Camilius Membe. Umekuwa na ari kubwa kukanusha kila suala la Tanzania linalojichomoza kimataifa. Unakanusha kila jambo hasa litangazwalo na vyombo vya habari vya kimataifa.

Ulianza na suala la Malawi kuhusu mpaka wa Ziwa Nyasa. Ukafuata suala la Balozi wa China aliyepanda jukwaa la CCM na kuhutubu. Tena,ukakanusha kuhusu ndege ya Rais wa China kubeba pembe za ndovu. Serikali yako pia ilikanusha kwa nguvu filamu ya Nightmare na uwindaji haramu.

Kubwa linaloisukuma Serikali ni kutangazwa habari zetu nje. Inadaiwa kuwa vyombo vya nje vinatuchafua na vina wivu. Sasa,nina taarifa kuwa kuna waandishi wa kimataifa wametinga Kiteto kurekodi dhahama ya kule. Wanatengeneza Documentary juu ya mauaji yanayoendelea Kiteto kati ya wakulima na wafugaji.

Wameshaanza kazi. Wanaendelea. Wakimaliza watatangaza mauaji hayo katika vyombo mbalimbali vya kimataifa vya habari kwa njia ya sauti na video. Nakuomba Waziri Membe uandae kanusho. Utalitumia punde. Usichelewe.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Mzee Tupatupa, heshima yako!!
Umeeleweka vyema.

Muda unakwenda kufichua mbao zilikwishaliwa na mchwa.
 
Hayo matatizo yangekua yanagusa familia ya rais ungekuta kisha kanusha.Membe na Sitta ni wanafiki sana
 
Hivi hili swala la kiteto kwa nini haliishi? kuna nini? anayelijua vizuri atuelezee vizuri hapa.
 
dah hiyo kweli mzee tupatupa kuna waandishi wanapiga mzigo kule uzuri wapo neutral nimewapenda sana waandishi Wa vyombo vya habari vya nje na tumewambia wawahi kuitoa ili serikali I take action nilipita hapo kiteto
 
Uongo naona ni sifa kubwa ya viongozi na wanasiasa (baadhi) wa nchi hii. Kibaya ni kuwa usipodanganya-kufanya makanusho kama Membe kura hupati.

Ugojwa huu ungeisha kupitia katiba mpya....lakini sasa kwa kuwa wakanushaji ni wengi wamelikomalia hilo ili katiba pendekezwa ipite kwa kulinnda upuuzi wa viongozi kama Membe itakuwavigumu kutoka hapa tulipo.

Labda niongeze tena ktk uzi wako juu ya Membe...'mtegeewa rais'.....alikanusha pia kuwa waasi wa Libya walikuwa kundi la majambazi waliotaka kuingusha serikali ya Ghadafi kwa kutumia pick ups na wasingeweza kumwondoa madarakani.

Sikumbuki pia kama alihusika kuhusu 'mapanki'...samaki wa Mwanza....minofu kuchukuliwa na wananchi kuuziwa mifupa.
 
Nilidhani umeandika namna gani ya kumaliza mgogoro wa kiteto kumbe unaandika kusifia wandishi wa kimataifa nenda na wewe wakakuhoji.
 
Nilidhani umeandika namna gani ya kumaliza mgogoro wa kiteto kumbe unaandika kusifia wandishi wa kimataifa nenda na wewe wakakuhoji.
kwani huwa mnazingatia mawazo ya wananchi?mambo mangapi mmeandikiwa hamtekelezi
 
dah hiyo kweli mzee tupatupa kuna waandishi wanapiga mzigo kule uzuri wapo neutral nimewapenda sana waandishi Wa vyombo vya habari vya nje na tumewambia wawahi kuitoa ili serikali I take action nilipita hapo kiteto

Yaani ni aibu sana,waandishi wetu wazalendo wamelala usingizi wakisubiri bahasha za khaki.Hivyo bado tupo mbali sana na hawa wazee wa bahasha.
 
Yaani ni aibu sana,waandishi wetu wazalendo wamelala usingizi wakisubiri bahasha za khaki.Hivyo bado tupo mbali sana na hawa wazee wa bahasha.


Wandishi wetu ndio walewale,bila bahasha za kaki maisha hayaendi mkuu.Ukizowea vya kunyonga...
 
Mauaji ya kiteto hayaigusi familia ya JK unafikiri watashughulika nayo?hapana
 
Mzee wa lumumba nakuunga mkono, ajiandae sawa sawa
 
Back
Top Bottom