Waziri Makamba: Umeme utaendelea kukatika mpaka tumalize maboresho. TPSF wamshukia kama mwewe

Kuna muda unajizuia usiongee lakini inakwaza.
Wananchi wako kimya, hawaoneshi kwa vitendo kusikitishwa na hali ya kukatika kwa umeme, maisha kupanda gharama katika nyanja zote.

Karibia kila kitu kinategemea umeme. Bila ya umeme hakuna ajira viwandani. Kuna kiwanda flani nakihifadhi jina, kimeshusha uzalishaji na kuondoa watu 120 kazini. Jambo baya sana.

Hawa watu 120 walikua na watu wengi sana nyuma yao wanawategemea. Watu hawa wanaishije? Watu hawa waliambiwa umeme ukikaa sawa wataitwa kazini, sasa ni kauli ya baada ya miaka 2.

Hivi watanzania, tuna akili timamu kweli? Mtu mmoja anajiita waziri, umeme ukatike usikatike auathiri mshahara wake, tunakubali kauli za kizembe namna hiyo.

Ifike hatua, nayeye awajibike. Umeme ukikatika, asilipwe mshahara. Kashindwa kusimamia wizara.

Bila nishati ya umeme hakuna maendeleo, taifa lolote lile.

Kwa kauli aliyotoa leo, ningekua mwenye nchi, ningetengua uteuzi wake.

Hopeless and rubbish.
Atafutwe mtaalamu wa umeme ndani ya shirika la tanesco, apewe wizara, tuone kama kutakua na shida. Mhandisi ana njia mbadala za kufanya kazi na matengenezo huku huduma ya umeme ikiwa palepale.

Watu wafanye marekebisho usiku, mchana uzalishaji viwandani uendelee. Watu wapate ajira, uchumi ukue.
Kalemani alikuwa mbobevu wa Sheria katika Nishati na Madini, yule Mkurugenzi wake wa Tanesco alikuwa mbobevu wa Electronic Engineering.

Sasahivi tuna mtu wa IT na yule muuza madishi ya DSTV ambae alimchagua yeye mwenyewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tumia akili sio hisia ,umeambiwa miaka 6 hakuna repair ilifanyika,umeambiwa uchumi wa ulikuwa umeanguka miaka ya Mwendazake hivyo mahitaji ya umeme yalikuwa chini na mwisho umeambiwa uchumi umeongezeka zaidi kwa hivyo loading imeongezeka na suluhisho ni kufanya repair na estimates zimewekwa.
Uchumi ulianguka mwa takwimu zipi? Word bank walitoa takwimu ya kupanda kwa uchumi, na serikali iliyopita uchumi wetu uliingia 'middle economy '

Mwanzo walisema umeme unakatika sababu ya ukame, mvua zikanyesha, akasema kutakua na 'scheduled maintenance ' ndani ya siku 10. Zikaisha siku kumi, na umeme bado unasumbua. Saiz wanasema maintenance itachukua 2 yrs. Kifupi ni siasa tu, wizara inababaisha.
 
Sasa hapo umetoka kwenye hoja umeanza matusi. Matusi nayajua sana,ila mimi sio kama wewe, najiheshimu. Napenda ninachokiweka humu mwingine akikipitia apate kitu. Ukishindwa hoja usilamishe wakuamini unachotaka kwa matusi.
Hawa watoto ndio hupewa posho za 10000 kwa siku kuja kulisha watu uongo, mfuatilie vizuri masaa 24 yupo humu, kwa kuongea pumba na mashudu. We pita kimya kimya acha wabaki wapumbavu.
 
Uchumi ulianguka mwa takwimu zipi? Word bank walitoa takwimu ya kupanda kwa uchumi, na serikali iliyopita uchumi wetu uliingia 'middle economy '

Mwanzo walisema umeme unakatika sababu ya ukame, mvua zikanyesha, akasema kutakua na 'scheduled maintenance ' ndani ya siku 10. Zikaisha siku kumi, na umeme bado unasumbua. Saiz wanasema maintenance itachukua 2 yrs. Kifupi ni siasa tu, wizara inababaisha.
Kama WB walitoa Takwimu za kupanda Kwa Uchumi ilikuaje ikatungwa sheria ya kuzuia kutoa Takwimu?

Kwani wewe hujui kwamba mwendazake alikuwa anapika Takwimu baada ya Hali kuwa mbaya?

Ndio maana sasa licha kupika Takwimu,Tanesco walionyesha mwenendo wa demand ya umeme ulionyesha kushuka sana so hata ukidanganya upande wa pili utaumbuka kwingine.

Takwimu zote zinaonyesha uchumi kushuka kuanzia kuporomoka kwa uwekezaji,kushuka kwa mahitaji ya umeme na kupora wafanyabiashara pesa,kubambikia matajiri Kodi na vitambulisho vya machinga.

Muulize Makamba ndio alitoa Chati ya mahitaji ya umeme miaka yote 6 iliyopita na Mwaka 2020/2021.

Mwisho nitafutie Takwimu na rekodi kama hii hapa kwenye mwaka wowote wa Mwendazake 👇

Screenshot_20220328-091139.png
 
Boss,
Uchumi umeongezeka maana yake matumizi ya umeme yame ongezeka, kama wateja wame ongezeka maana yake mitambo yetu inatakiwa iongezewe capacity kukidhi ongezeko la watumiaji, kama kweli ni hivyo basi Tanesco wana takiwa ku upgrade mitambo Yao ya awali Kwa kuiongezea uwezo zaidi na kupanua njia za usafirishaji, hii ni kuangalia tufanye nini katika mitambo yetu ya sasa kuongeza uzalishaji sio ku repair , repair haiongezi uzalishaji wa umeme na haina uhusiano na uchumi.

Pili kama mitambo haiwezi kuwa upgraded na Kuna capacity limitations kifuatacho ni kufanya nini expansion, expanding uzalishaji wa umeme Kwa kujenga vituo vipya vikubwa au vidogo kwa haraka Kwa matumizi ya sasa na miaka ijayo kadri ya ongezeko la mahitaji,sasa new build takes time, inahitaji pesa lakini ni solutions ya kudumu zaidi kuliko njia zingine, ndio maana Kuna ujenzi wa kinyerezi 1,2,3,4 na kuendelea, ndio maana Kuna stieglers, Kuna solar energy, makaa ya mawe na etc.

Repair ni aibu hata kusema kuwa wakirepair uzalishaji utaongezeka, ni aibu kubwa Kwa Tanesco na waziri kutoa taarifa ambayo hawajui maana yake nini, chukua mfano, una daladala yenye abiria 10, lakini unapofika kituoni una kuta Kuna abiria 20, hivyo una beba abilia wako 10 na wengine kuwaacha, so ukitaka kuwabeba abiria wote utapeleka gari lako likafanyiwe repair ? Jibu ni no, Bali utafanya yafuatayo;

1. Expansions Kwa kuongeza seat ya abiria kama gari lina nafasi, kama halina una weza hata fumua bodi ukaongeza ili upate nafasi.
2. Baada ya kuongeza nafasi, fumua bodi,je engine uwezo wake utafaa? Kama engine capacity ni kidogo una upgrade.

3. Suluhisho la kudumu ni kununua daladala ya pili iweze kubeba hao abiria wengine (new build).

Matengenezo hayaongezi uzalishaji na kukidhi mahitaji ya umeme hapo Tanesco wana paka ragi upepo, hakuna jitihada wanazifanya zaidi ya kutokili kuwa wamefail na wana mshauri vibaya waziri, makamba sio mtalaamu wa umeme na hajui anacho ongea, yeye anatakiwa awabane Tanesco waache kutoa sababu za uongo Bali wajikite kutafuta njia mbadala na kuondokana na tatizo hilo,waache kukaa ofsini wakisubiri tatizo ,

Tanesco nadhani utendaji ni mbovu watu wanafanya kazi Kwa mazoea.
Mi naona anatulia timing tu arudishe "Service Charge"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanzania uliingia uchumi wa Kati toka 2016 bali ilikuwa kwenye kipindi cha matazamia,kwa muktadha huo uchumi ulipungua Kasi ya kukua lakini haukuanguka kabisa so ile range ya per Capita ikawa sustainable.

Naona wazee wa legacy mumebakia na hako ka uchumi wa Kati kujitetea, Uchumi wa Kati tukifika toka enzi za JK.
2016 JK ndio alikua madarakani? Pombe gani za asubuh hizi?
 
Pamoja na mipango mibovu ya awali amesema pesa za matengenezo zinazohitajika ni til.4 na wamepata bil.400 tuu ndio msingi wa kwamba haijulikani umeme utaacha lini kukatika.

Kwa hiyo wewe unadhani shida ni nini kama.sio pesa za kufanyia matengenezo?

4 triliion anataka kuanzisha tenesco mpya au
 
Back
Top Bottom