Waziri Kombo amuaga Balozi wa Angola

Waziri Kombo amuaga Balozi wa Angola

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,770
Reaction score
1,173
WAZIRI KOMBO AMUAGA BALOZI WA ANGOLA

Balozi wa Angola anayemaliza muda wake, Mhe. Sandro De Oliveira amekutana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb) kwa madhumuni ya kuaga.

Katika kikao hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam Juni 21, 2025, Mhe. Balozi Sandro De Oliveira alitumia muda huo kuishukuru Wizara na Serikali kwa ujumla kwa kumpa ushirikiano uliomuwezesha kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi katika kipindi chote cha uwakilishi nchini.

Viongozi hao pia walijadili masuala mbalimbali ya kisekta kuhusu ushirikiano kati ya nchi ya Tanzania na Angola, ikiwemo sekta ya Gesi na Mafuta, Madini, Uchumi wa Buluu, usafirishaji kwa njia ya reli na Ushoroba wa Lobito.

IMG-20250622-WA0066.jpg
IMG-20250622-WA0077.jpg
IMG-20250622-WA0075.jpg
IMG-20250622-WA0067.jpg
IMG-20250622-WA0063.jpg
IMG-20250622-WA0068.jpg
 

Attachments

  • IMG-20250622-WA0060.jpg
    IMG-20250622-WA0060.jpg
    252.2 KB · Views: 22
  • IMG-20250622-WA0062.jpg
    IMG-20250622-WA0062.jpg
    299.6 KB · Views: 19
Back
Top Bottom