mkiluvya
JF-Expert Member
- May 23, 2019
- 802
- 725
Amesema tangu kuingia Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli yamefanyika mabadiliko mbalimbali yaliyolenga kuleta tija na kuifungamanisha sekta ya utalii na maendeleo ya watu kwa kuhakikisha wananchi wananufaika na sekta hiyo.
Dkt. Kigwangalla amesema Serikali ilifanya jitihada za makusudi za kulegeza masharti na kushusha viwango vikubwa vya tozo vilivyokuwepo ambavyo vilikua vinawazuia wafanya biashara wadogo hasa wazawa washindwe kuingia katika sekta hiyo. Amesema tangu kuondolewa kwa masharti hayo watanzania wazawa wanaofanya biashara ya huduma za utalii wameongezeka kutoka 1100 hadi kufikia 2000 wengi wao wakiwa watanzania.