Jana Waziri George Huruma Mkuchika, Waziri katika Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora alitoa ufafanuzi kuhusu hoja za Wabunge wa Upinzani na CCM kuhsu watu kutekwa, kupotezwa au kushambuliwa mchana kweupe na Mwandishi wa Habari Bwana MUSIBA anavyotoa matamko ya KICHOCHEZI lakini TISS wamekaa kimya.
Waziri katika kama kawaida ya Serikali ya CCM Kajibu hoja zote kisiasa na propaganda nyingi zenye kupotosha. Kwa kifupi niseme alichofanya Mkuchika ni KUJIBU HOJA NZITO KWA MAJIBU MEPESI,YA KITOTO NA YENYE KUPOTOSHA.
Mkuchika anawatetea TISS au UWT(Usalama wa Taifa) kwamba ATI TISS HUFANYA KAZI ZAO KIMYAKIMYA NA KUSHAURI SERIKALI NINI CHA KUFANYA. Huu ni uongo wa mchana kweupe. Usalama wa Taifa ya sasa kiukweli hawa ni USALAMA WA CCM na Serikali yake. TISS wako kutetea CCM na kukandamiza, kuonea, kunyanyasa na kuua Wapinzani kwa MASLAHI YA CCM NA SERIKALI YAKE.!!!
Kama kweli TISS wanafanya kazi kwa weledi unaostahili kama TISS ya enzi za Baba wa Taifa tusingelikuwa tunasikia upuuzi unaofanyika kwa sasa hapa Tanzania. Watu wameuawa huko Kibiti kwa karibu mwaka mzima na TISS wapo tu. Watu wakihoji kwanini watu wanauawa Waziri Daktari uchwara Nchemba anasema INAWEZEKANA CHADEMA wanahusika maana haiwezekani watu wa chama fulani(CCM) peke yao ndio wanauawa lakini Upinzani hawauawi...!!!Je, TISS walikuwa wapi kujua kuwakamata hao CHADEMA au CUF au ACT-Wazalando ili dunia ijue kwamba kumbe vyama vya upinzani ni vyama vya KIGAIDI??
Wakati Mkuchika anadanganya watu kwamba UWT wanaendelea kufanya kazi zao kimyakimya, i hali halisi ni tofauti kabisa na kinachotokea kwenye eneo la tukio.. Kuna Polisi 8 huko Kibiti na mpaka leo hatujui nani walihusika..?TISS wanafanya kazi kimyakimya.....Kuna mwandishi Azory Gwanda ametoweka kutoka eneo la tukio(KIBITI) akiandika habari za Kiuchunguzi kuhusu Mauaji hayohayo na mpaka leo zaidi ya siku 100 Gwanda hajaonekana....LAKINI TISS WANAENDELEA KUFANYA KAZI KIMYAKIMYA...!!
Kuna Ben Saanane ametoweka huu ni mwaka wa pili na haijulikani yuko wapi na nani aliyemteka. Watu wakihoji wanaambiwa waulizwe CHADEMA maana wanajua alipo...??TISS wapo tu wanaendelea kufanya kazi kimyakimya...!! Tundu Lissu kashambuliwa kwa Risasi zaidi ya 30 kwenye maeneo ya Bunge tena Makazi ya Viongozi wa Serikali na Waheshimiwa Wabunge mpaka leo hakuna hata sisimizi wa kusingiziwa amekamatwa....TISS WAPO WANAENDELEA KUFANYA KAZI YAO KIMYAKIMYA......!!!
Mwanafunzi wa NIT kauawa kwa kupigwa risasi na Polisi waliokuwa wanataka kuwazuia/kuwaua Viongozi wa CHADEMA waliokuwa wanakwenda kwa Mkurugenzi wa Kinondoni kuadai Viapo vya Mawakala kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi...Leo Viongozi wa CHADEMA ndo wanaambiwa wanahusika na kifo cha Acqulina Akwiline.....Kwa maana nyingine Mbowe na wenzake ndio walifyatua risasi za kumwua Acqulina....Polisi waliokuwa na silaha za moto , Kamanda Mambosaasa aliyaamrisha Polisi wafyatulie risasi za moto watu wasiokuwa na hatia na Mkurugenzi wa Kinondoni hawahusiki kabisa kwa lolote....TISS WANAENDELEA KUFANYA KAZI KIMYAKIMYA....!!!
Kwa Waziri Mkuchuchika na CCM watu kuendelea kupotea, kuuawa, kushambuliwa na wapinzani kukamatwa, kufunguliwa mashtaka na kesi za hovyohovyo ndiyo UTAWALA BORA wa CCM na Serikali yake huku TISS au UWT wakiende;ea kufanya kazi kimyakimya......!!!
Hitimisho ni kwamba TISS wataendelea kufanya kazi zao kimya kimya huku wakiendelea kupanga mikakati ya kuwapoteza, kuwashambulia au kuwamaliza kabisa Viongozi wote wa Upinzani kimya kimya maana ndiyo kazi ya TISS kwa sasa na huo ndiyo utawala bora...!!!