Ukitoa uchovu, tabia zako za kila siku kwenye udereva zinakuathiri popote pale. Mtu anaeendesha hovyo hovyo mjini hata ukimkuta highway ana tabia hizo hizo ndio maana kuna ajali nyingi za kizembe.
Kabisa. Nikionaga watu wa IST na Crown walivyo na fujo mijini, uwa nasema hawa ndiyo wanaokula mizinga ya kijinga highway. Unakuta mtu yupo mjini ana-overtake kijingakijinga - yupo upande wako na ati anakuwashia taa! Uwa nawapisha, ila mtu wa namna hiyo highway lazima aingie chini ya kichanja kwa uendeshaji huo!