Wazee wa Dar: Tulitaka kumuuliza Rais

Wazee wa Dar: Tulitaka kumuuliza Rais

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Wamelalamika kuwa wao hawakuuliza. Wanasema kama kuzungumza nao,kama inavyokuwa kwa Waandishi wa Habari,walikuwa na shauku ya kurusha maswali yao kwa Rais baada ya hotuba yake.

Wanalalamika kunyimwa nafasi. Wengine wameapa kutokwenda tena watakapoitwa. Nimejaribu kuwaelewesha bila ya kueleweka na wao kuelewa. Wakatest kuniuliza maswali mawili-matatu.

La kwanza,kwanini TANESCO hawakurudi ICSID kwa miaka saba na wakuu wao,yaani Wizara ya Nishati na Madini, kutowahoji kwa kutokwenda kwao huko? La pili,mgogoro kati ya TANESCO na IPTL ulikuwa ukijulikana Serikalini?

La tatu,ni kweli kulikuwa na hukumu iliyoamuru fedha zilipwe kwa IPTL? CAG alikagua vipi fedha isiyo ya umma? La tano,kukiuka kulipa kodi kunasameheka na si jinai tena?

Kutokana na uzito wa maswali hayo,kulingana na umri na uwezo wangu,nimewaomba niwajibu kwa barua au simu baada ya utafiti ulio fiti.

Rais anaweza kufikishiwa maswali haya. Ni ya msingi!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Wazee wenyewe vilaza kama bosi wao. Ndo maana wanapelekeshwa utadhani wamekatwa vichwa.
 
Mnalo na mengi wako eti na wewe unataka kugombea ubunge pwani atakuchagua binamu yako na wale wenzako pale mlimani.
 
Ukweli hotuba yake itaibua mambo mengi ambayo majibu bado ni kitendawili.
 
Ni kweli Mkuu ashinikizwe huyu DHAIFU kwamba hotuba yake imeacha maswali mengi sana kuliko majibu. Tunataka aitishe news conference ili ajibu maswali husika toka kwa waandishi wa habari bila kukwepa na kujichimbia Ikulu.

Ukweli hotuba yake itaibua mambo mengi ambayo majibu bado ni kitendawili.
 
Mzee Tupatupa, Rais ameyasikia maswali ya "wazee wa Dar es salaam" ila majibu yao yatategemea uchunguzi unaoendelea.

Isipokuwa mimi nina neno kwa wabunge wetu , sasa ndo muda maalumu wa kupiga kura ya kutokuwa na imani na Pinda hakuna kurudi nyuma mpaka JK arudi kutekeleza maamuzi yote ya bunge. Nakumbuka Pinda aliahidi kuwa atahakikisha maazimio yote ya bunge yanatekelezwa. Huyo ndo wa kula kichwa, bila hivyo bunge letu litazidi kudharauliwa. dawa ndo hiyo nawapeni mg'ang'anieni Pinda ang'oke lazima serikali yote itawapigia magoti tu.
 
Ki ukwel hayo maswali hakuna wa kuyajibu katika serikali hii akitokea wa kuyajibu CCM itatawala milele
 
we kiboko amakyasa nilimaanisha hawa wadada upo smart sana .na wewe umezijuaje hizi dizaini utakuwa mzee wa east africa wewe

Nilikuwa makini sana kuwaangalia hao wanaoitwa wazee wa darisalama. Hiyo picha nimepost hata kule jamii forum photos nimeuliza : Hivi hawa nao ni wazee wa dar es salaam?
 
hao wazee wanaolazwa majumbani kwao saa kumi na mbili jioni na panya road ndio wangethubutu kumhoji rais hayo maswali.?
 
Kitendo Cha kumuacha mpasua miamba wizarani ni kosa kubwa sana JK atolisahau.
 
Hakika leo Rais ameongea maneno yasiyo fanana na ofisi yake na taasisi lukuki allnazozisimamia tena za wataalamu wa kutosha, Rais unasoma maazimio ya Bunge kwa kejeli?, Rais unafafanua kitu ambacho kilishafafanuliwa zamani na kueleweka kwa watu?, Rais kila majibu yako yanasingizia uchunguzi unaofanyika tuuuuuu na toka lini mtu akachunguzwa akiwa ofisini tena akiwa anajua kuwa anachunguzwa?,

Ndugu Rais yaani umekuwa kama Ibilis(najua wewe Muislam) yaani alikuwa akifanya mazuri na mema sana akapata sifa alafu akaharibu kwa tendo moja tu uongozi wako wote umeutia kinyesi hadharani, Rais hivi hiyo bajeti ijayo utaipitisha kwa njia gani bunge lijalo, vipi utatumia vikao Vya chama?. Na eti uliwashangaa wabunge wa ccm ambao hawakukataa uovu bungeni? Sasa kama unakiri kuwa ulikuwa uovu mbona huchukui hatua?

Nawasihi wabunge wetu wasiwe mihuri ya kilinda uovu
 
Swali langu ni kwa nini ukubali pesa yenye mgogoro upande mmoja ukijua kuwa hawa watu hawajakubaliana yaani Iptl na TANESCO. Lingine nani alishauri kuanzishwa escrow a/c kwa maelezo ya rais baraza lake la mawaziri walikuwa wanajua kuhusu jambo hili
 
Wamelalamika kuwa wao hawakuuliza. Wanasema kama kuzungumza nao,kama inavyokuwa kwa Waandishi wa Habari,walikuwa na shauku ya kurusha maswali yao kwa Rais baada ya hotuba yake.

Wanalalamika kunyimwa nafasi. Wengine wameapa kutokwenda tena watakapoitwa. Nimejaribu kuwaelewesha bila ya kueleweka na wao kuelewa. Wakatest kuniuliza maswali mawili-matatu.

La kwanza,kwanini TANESCO hawakurudi ICSID kwa miaka saba na wakuu wao,yaani Wizara ya Nishati na Madini, kutowahoji kwa kutokwenda kwao huko? La pili,mgogoro kati ya TANESCO na IPTL ulikuwa ukijulikana Serikalini?

La tatu,ni kweli kulikuwa na hukumu iliyoamuru fedha zilipwe kwa IPTL? CAG alikagua vipi fedha isiyo ya umma? La tano,kukiuka kulipa kodi kunasameheka na si jinai tena?

Kutokana na uzito wa maswali hayo,kulingana na umri na uwezo wangu,nimewaomba niwajibu kwa barua au simu baada ya utafiti ulio fiti.

Rais anaweza kufikishiwa maswali haya. Ni ya msingi!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Huyu Zombie nilijua leo ana conclude hii saga yeye kaianzisha upya sasa mfikishieni ujumbe tunataka majibu ya haya maswali. Alibembeleza wezi wa EPA sasa hawa wa ESCROW pia anataka kuwabeba safari hawa lazima adondoke nao.
 
Tumbili kashafukuza Mwizi, Sasa Mwizi Mkuu anavilinda vijizi vidogo. Alitakiwa atumie advantage ya Mwizi Tumbili naye afukuzie hapo.
 
wale walikuwa wazee feki wa dar wale ni wazee wa east africa ingawa kulikuwa na mashangazi wa chalinze msoga

Wazee walioandaliwa na sare za chama chao cha mafisadi? Inawezekana ndio sababu ya rais kuahirisha kukutana nao ijumaa iliyopita kwani inawezekana sare hazikuwa tayari.
 
Mzee tupatupa msijadili chama mfu tumesha ki delete ccm siku mingi sana
 
Back
Top Bottom