Wamejaa hekima kuliko wazee wote wa Tanzania
Ni wasikivu hata raisi wetu anajivunia
Sio wabishi kila wanachoambia wanasikia
Ni wataratibu hata ukiwatukana watakushangilia
Watakupigia makofi bila kujali unachoongea
Hata kama unataka kuua baraka watakupatia
Wana uelewa mkubwa wa kila jambo linalotokea
Wanatumika kama chombo matamko kuyatolea
Busara na hekima zao hakuna mfano wa kupigia
Akili za kuambiwa pia zao wamechanganyia
Wazee wa mikoani usia nawapatia
Msiwe wabishi mtazidi kujiaribia
Hasa nyinyi wa kaskazini na wenzenu wa mbeya
Hizo people people wakuu hawataki kuzisikia
Mmevuka mipaka mmewaambukiza na wa kanda ya ziwa
Mnatuharibia vijana rangi zetu wanazichukia
naomba niishie hapa tamati nimefikia
Mwenye akili timamu ashaelewa nnachoongea
Ni wasikivu hata raisi wetu anajivunia
Sio wabishi kila wanachoambia wanasikia
Ni wataratibu hata ukiwatukana watakushangilia
Watakupigia makofi bila kujali unachoongea
Hata kama unataka kuua baraka watakupatia
Wana uelewa mkubwa wa kila jambo linalotokea
Wanatumika kama chombo matamko kuyatolea
Busara na hekima zao hakuna mfano wa kupigia
Akili za kuambiwa pia zao wamechanganyia
Wazee wa mikoani usia nawapatia
Msiwe wabishi mtazidi kujiaribia
Hasa nyinyi wa kaskazini na wenzenu wa mbeya
Hizo people people wakuu hawataki kuzisikia
Mmevuka mipaka mmewaambukiza na wa kanda ya ziwa
Mnatuharibia vijana rangi zetu wanazichukia
naomba niishie hapa tamati nimefikia
Mwenye akili timamu ashaelewa nnachoongea