SautiYaMnyonge
JF-Expert Member
- May 13, 2018
- 439
- 742
Kirua Vunjo Kusini.
Koresa.
Tarehe 10/12/2021.
Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mhe. Dkt. Charles Kimei amekutana na Wazee mashuhuri kutoka Kata ya Kirua Vunjo Kusini waliomualika kuzungumza nao.
Wazee hao wakiongozwa na Mzee Gasper Ngowi walimweleza Mhe. Mbunge dhamira yao ya kuanza kujenga Kituo cha Afya kwa michango yao binafsi ili kuhudumia wananchi. Mzee Ngowi kwa niaba ya wazee wenzake wamemtaka Mhe. Mbunge kuendelea kuchapa kazi ili kumsaidia Mhe. Rais na kumtaka aendelee kutenda zaidi aliyotumwa na wananchi wake.
Wamemhakikishia kumuunga mkono katika dhamira yake ya kuleta Maendeleo Jimbo la Vunjo na wanaridhishwa na kazi kubwa anayoifanya kwa sasa. Wamemueleza asihofu wala kukata tamaa maana wao waliompa dhamana hiyo wanaridhishwa na kazi waliyomtuma.
Mhe. Mbunge, amewashukuru kwa kuendelea kumpa imani, amewaahidi kutowaangusha katika kuleta Maendeleo ya Jimbo la Vunjo. Mhe. Mbunge amewataka kuendelea kumuombea kwa Mungu ili kazi hii ya kuwatumikia wananchi aifanye vizuri zaidi.
Mhe. Mbunge amewachangia Tsh Milioni 2 ili kumalizia Ujenzi wa Ofisi ya Kijiji.
VUNJO KAZI INAENDELEA.
Koresa.
Tarehe 10/12/2021.
Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mhe. Dkt. Charles Kimei amekutana na Wazee mashuhuri kutoka Kata ya Kirua Vunjo Kusini waliomualika kuzungumza nao.
Wazee hao wakiongozwa na Mzee Gasper Ngowi walimweleza Mhe. Mbunge dhamira yao ya kuanza kujenga Kituo cha Afya kwa michango yao binafsi ili kuhudumia wananchi. Mzee Ngowi kwa niaba ya wazee wenzake wamemtaka Mhe. Mbunge kuendelea kuchapa kazi ili kumsaidia Mhe. Rais na kumtaka aendelee kutenda zaidi aliyotumwa na wananchi wake.
Wamemhakikishia kumuunga mkono katika dhamira yake ya kuleta Maendeleo Jimbo la Vunjo na wanaridhishwa na kazi kubwa anayoifanya kwa sasa. Wamemueleza asihofu wala kukata tamaa maana wao waliompa dhamana hiyo wanaridhishwa na kazi waliyomtuma.
Mhe. Mbunge, amewashukuru kwa kuendelea kumpa imani, amewaahidi kutowaangusha katika kuleta Maendeleo ya Jimbo la Vunjo. Mhe. Mbunge amewataka kuendelea kumuombea kwa Mungu ili kazi hii ya kuwatumikia wananchi aifanye vizuri zaidi.
Mhe. Mbunge amewachangia Tsh Milioni 2 ili kumalizia Ujenzi wa Ofisi ya Kijiji.
VUNJO KAZI INAENDELEA.