Wazazi wamshtaki mtoto wao wa kiume ambaye amekataa kuhama nyumbani

Kaka Pekee

JF-Expert Member
Apr 3, 2018
336
559

Wazazi wa mwanamume mmoja wa umri wa miaka 30 wametumia mbinu zisizo za kawaida kumlazimisha mto wao huyo kuhama nyumba yao.

Nyaraka za mahakama zinasema kuwa Michael Ratondo halipi kodi ya nyumba wala hasaidii na kazi za nyumbani na amepuuza msaada wa kifedha wa wazazi kutaka kumwezesha apate nyumba yake ya kuishi.

Licha ya kumuandia barua mara tano kumtaka ahame nyumba yao Christina na Mark Rotondo wanasema mtoto huyo wao amekataa kuhama.

View attachment 784886
Michael Rotondo (30) (pichani) ndiye jamaa aliyetimuliwa na wazazi wake kwa kutofanya kazi yeyote na kuendelea kung'ang'ania kuishi nyumbani kwao.

View attachment 784887
Wazazi wa Kijana Michael na Picha ya chini ni nyumbani kwao alipokuwa akiishi na wazazi wake hao.
View attachment 784888
Michael-Rotondo6.jpg

Michael anasema kisheria hakupewa muda wa kutosha kumwezesha kuondoka.

Bi na Bw Ratondo walipeleka kesi kwenye mahakama ya Onondaga karibu na Syracue, New York tarehe saba mwezi Mei baada ya miezi kadhaa ya jitihada za kumshawishi mtoto huyo kuhama kufeli.

"Tumeamua kuwa ni lazima uondoke nyumba hii mara moja," barua moja iliyokuwa imeandikwa Februari tarehe 2 ilisema.

Wakati Michael alipuuza barua hiyo, wazazi wake waliandika tena barua ya kumuagiza ahame kwa msaada wa wakili wao. Source: Bbc Swahili Wazazi wamshtaki mtoto wao kwa kukataa kuhama nyumbani
 
mtoto wa kiume ahame aende wapi?wa kike sawa anaolewa,wa kushtakiwa ni wazazi bwana kwa kushindwa kumjengea mtoto wao nyumba,
 
hahahahhah dah . wanataka aende wapi sasa wakati hapo ndo kwao, ila wazungu wapo real saana , ila kwa wazazi wetu ingekua visa tu kwanza
 
Hao wazazi wanamuonea huyo kijana,waje tz watamkuta mzee wa miaka 54 alikua analala sebuleni kwao mpka akafukuzwa almaarufu le mbebez
 
unamuacha tu,kama umejenga kwingine unamuacha hapo wewe unasogea pembezoni,au unamjengea atulie kwa nini ahangaike na nyumba ya wazazi ipo kodi inaumiza sana,aisee mimi kidume wangu atakaa home mpaka atakapopapa mjengo wake au nimpe wake,tena sababu ni mwanaume hata ukijenga pembeni jenga nyumba ndogo kwa ajili yake,ya nini kuwatesa watoto hela anazotafuta afanyie mengine si kulipa kodi bana na nyumba ipo
Jitu zima linang'ang'ania nyumbani? Mtakua wafugaji wa binadamu
 
Jamaa anawanyima wazazi muda wa kuserebuka.wao wanatamani wasex hata sittin room lakin ndo hivyo mtoto yupo
 
mtoto wa kiume ahame aende wapi?wa kike sawa anaolewa,wa kushtakiwa ni wazazi bwana kwa kushindwa kumjengea mtoto wao nyumba,

Desturi za wazungu between 18-22 years kijana lazima ahame nyunbani aanze maisha yake. Wewe unareason kama mwafrika kwamba kijana atajenga nyumbani. Hiko ulaya hata kuridhi wazazi wako sio haki yako. Wakipenda wataandika will mali yao iende kwa mashirika ya kijamii.
 
Wewe umeongea maana nlijua mila zetu mwe mwe mwe
Desturi za wazungu between 18-22 years kijana lazima ahame nyunbani aanze maisha yake. Wewe unareason kama mwafrika kwamba kijana atajenga nyumbani. Hiko ulaya hata kuridhi wazazi wako sio haki yako. Wakipenda wataandika will mali yao iende kwa mashirika ya kijamii.
 
Back
Top Bottom