Mgunyamweusi
Member
- Dec 19, 2012
- 19
- 1
Katika hali ya kawaida ya kuhabarishana na kufurahishana rafiki yangu mmoja ametumia picha hiii. Na nikaona si vibaya nikawashirikisha nanyi ndugu zangu ili tupate cha kujifunza.
Imekuwa ni kawaida kwa wazazi wengi inapotokea kutokuelewana, basi hugombana na kutoleana maneno mazito bila kujali uwepo wa watoto wao.
Jambo ambalo huwajenga watoto kuwa na hisia mbaya hisia ambazo haziwezi kufutika akilini mwao kwa haraka. Pia hisia hizo huenda zikapelekea watoto hao kuwa na tabia zisizokubalika katika jamii hapo mbeleni.
Kutokana na Picha hii nimejifunza kuwa, Ndugu zangu, inapotokea kutokuelewana baina yetu kama wazazi au wapenzi basi mambo haya tuyafanye katika mazingira ambayo hayawezi kuwaaathiri watoto wetu.
Wana jukwaa wenzangu mna mtazamo gani katika hili?
Nawasilisha
Imekuwa ni kawaida kwa wazazi wengi inapotokea kutokuelewana, basi hugombana na kutoleana maneno mazito bila kujali uwepo wa watoto wao.
Jambo ambalo huwajenga watoto kuwa na hisia mbaya hisia ambazo haziwezi kufutika akilini mwao kwa haraka. Pia hisia hizo huenda zikapelekea watoto hao kuwa na tabia zisizokubalika katika jamii hapo mbeleni.
Kutokana na Picha hii nimejifunza kuwa, Ndugu zangu, inapotokea kutokuelewana baina yetu kama wazazi au wapenzi basi mambo haya tuyafanye katika mazingira ambayo hayawezi kuwaaathiri watoto wetu.
Wana jukwaa wenzangu mna mtazamo gani katika hili?
Nawasilisha