MESAYA
Member
- Jan 4, 2012
- 55
- 52
Kama ni kuzindisha uchungu kwa serikali yangu basi hili limeongeza mara tatu zaidi ya ilivyokuwa awali. Katika Bunge lililopita Mh Magembe alikiri bila aibu kamba wawekezaji wa mashamba hapa Tanzania wanalipa Tsh 200 kwa mwaka. Lingine ni hili la sukari kwamba gharama za uzalishaji wa sukari hapa kwetu ni Tsh 1200 ila kinachosababisha bei kuwa juu ni toza sa serikali. sasa cha kujiuliza ni kwamba:
- Je watanzania wanashindwa kukodi mashamba haya na kutumia kuzalisha chakula cha kuwalisha watanzania au kuna mtu fulani anafaidika kupitia mradi huu?
- Je serikali haioni kwamba kuna ulazima wa kutoa ruzuku kwa viwanda vya sukari na kuondoa tozo ili bei ya zao hili lishuke mpaka bei ya kuzalishia ili watanzania waweze kumudu kuliko ilivyo sasa?
- Kwa mantiki hii si shairi kwamba serikali haina nia ya kuwasaidia watanzania na kuijenga Tanzania bali kujisaidia wao wenyewe na kujenga maslahi zao binafsi?