Mashabiki wa Yanga na Simba ni mashabiki wa timu mfu ambazo akili zao zinaongozwa na watu wachache na wao mashabiki wanashabikia kama vipofu. Viongozi wao hata waibishe vipi bado mtakuja kuwashabikia hapa. kulikuwa na haja gani kwa timu ya Yanga kupeleka timu Kigali kwa ajili ya kufanya tathmini ya timu yao kabla ligi haijaanza?? maximo anafahamu angepeleka timu yake halafu afungwe akifukuzwa kama mbwa mwizi kwa hiyo akaamua kwenda pemba na kucheza na timu za mchangani na bado mashabiki maandazi wa yanga mkashangilia.
Timu zenu kongwe za yanga na simba hazijafanya lolote la maendeleo bado mnawashabikia tu. hawana viwanja, hawana gym ya mawazo, hawana hosteli, hawana swimming pools wala kitu chochote cha maendeleo lakini bado mnawashangilia viongozi wenu ambao wamewashikia akili.
Mnatakiwa kuelewa kwamba Azam ndio mabingwa wa Tanzania mpaka mwisho wa msimu na lazima mashabiki wa simba na yanga muonyeshe heshima kwao.
Mpira wa Tanzania utakuwa kama ligi kuu itapata hatua kama tutapata timu mbadala wa yanga na simba. yanga na simba ni failures ambao hawawezi kupiga hatua yoyote ya kimaendeleo