Wauza machungwa na uchafu

Godwin peter

JF-Expert Member
May 12, 2019
360
605
Mara nyingi jioni nikitoka kwenye mishe zangu napita kwa jamaa mmoja anauza machungwa nakula chungwa zangu kama tano hivi ndo nasepa geti

Sasa leo nimepita nikachukua chungwa kama tano hivi nikakaa hapo hapo taratibu nikaanza kula sasa baada ya muda kidogo alikuwa anajukuna kwenye makalio tena ndani ya boxer yaani nilijisikia hovyo kweli yaani hadi tumbo likawa linauma….uchafu tunaokula sio poa.
 
Mara nyingi jioni nikitoka kwenye mishe zangu napita kwa jamaa mmoja anauza machungwa nakula chungwa zangu kama tano hivi ndo nasepa geto…Sasa leo nimepita nikachukua chungwa kama tano hivi nikakaa hapo hapo taratibu nikaanza kula sasa baada ya muda kidogo alikuwa anajukuna kwenye makalio tena ndani ya boxer yaani nilijisikia hovyo kweli yaani hadi tumbo likawa linauma….uchafu tunaokula sio poa.
Nunua chungwa fresh Nenda nalo home uoshe na kumenya mwenyewe.
Hata ukiosha na sabuni au maji moto ni wewe tu
 
Yaani kuna mahali nilikuta wanaosha na sabuni ili eti yang'ae..
20230711_012935.jpg
 
Wengine unakuta anajikuna pumb.u halafu anajinusa kwanza yeye mwenyewe.
Juzi jumapili tulikaa watatu kijiwe fulani, mmoja wetu akaagiza embe kwa muuzaji wa jirani amletee embe moja amenye kabisa.
Muuza akalimenya safi na mikono yake halafu akamwagiza mwanae wa miaka kama 7, naye kwa mikono miwazi hivyo hivyo akalileta.

Jamaa mwenzetu akamchana live kwamba wenzako embe la kumenywa huwa hawashiki na mikono wanakuwa na vikaratasi, sasa wewe umeshika na mikono kuanzia wewe mwenyewe halafu unamwagiza na mwanao na mikono hivyo hivyo, kuleni wenyewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom