Waunguja wawabagua Wapemba

matongo

New Member
Mar 16, 2011
4
4
Vipeperushi hivi vimesambazwa kwa kasi jana katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar vikiwa na ujumbe unaowataka Wapemba waondoke Unguja na kurudi kwao Pemba wakajipange huko kuukataa Muungano.

Sehemu ya waraka huo - angalia kiambatanisho....

UPDATED:

 

Attachments

  • Waraka kwa Uamsho.pdf
    29 KB · Views: 1,492
fitna hizi.. na uzushi... sidhani kama wazenji ndio wameandika huu...





 
Nyerere alisema jeuri ya wazanzibar kujiita wazanzibari, inatokana na muungano. Pasipo muungano hakutakuwa na Zanzibar, badala yake kutakuwa na Unguja na Pemba. Hizi ni dalili tosha kwamba baada ya muungano kuvunjika, watabaguana tena. Kama nia yao ni kuikataa bara, kwanini wasiungane pamoja bila kujali uunguja na upemba kuikabili Tanganyika?
 
safi sana maana haiingiii akilini wabara wafukuzwe pembe ili hali wapemba wapo kibao huku bara
 
hahahah hii itakuwa ni janja ya ccm!
Basi waziri mkuu tuwe tunamchagua wenyewe wa tanganyika aaati!
 
Sasa kule ambako kila mtu alikua anategemea ndio tunaelekea,

Hawa pimbi wabaguzi sana!
 
Hata bila kijiujumbe hiki, ukweli ni kwamba huko ndo wataelekea. Ndo gharama ya upumbavu.
 
Mh ! huo ni uongo kabisa, ni hila za kisiasa na kutaka kuwadhoofisha wadai haki yao ya muungano! msirudi nyuma vijana ! endeleeni kudai haki yenu ni muungano gani mnautaka ! dunia sasa hivi watu wameamka sio mambo yale ya kizamani jamani!
 
Mtalaaniwa hii ni propaganda ya ubaguzi sidhani kama Pemba na Unguja imefikia hatua hivyo,,,,, acheni kuongeza machungu kwa watawala
Gaadem! nyie mkijua upande huu na wenzenu wanajua upande wa pili...sasa hapa ni full propaganda chezea wabara wewe!
 
1. Sasa hapa sisi Watannganyika tuendelee kuwauliza tu consistently mpaka waseme khaswaa wanataka nini kwa vurugu hii??
2. Kama wahuni ....kama wanafahamu na lengo hiyo juu yao sisi letu moja tu WANATAKA NINI HAWA??? Na wamatumwa na kupata nguvu kutokea wapi????
3. Na kama hayatatoka maelezo ya kina then hili tatizo litakuwa relapsing and persistent cum intermittent in character

Tusikubali haya maneno kama ya khanga hayana authority wala responsibility kama wanayamaanisha waweke adress zao tuhoji zaidi............ let us face the problem and dig the roots up !!!!!!
 
Mh ! huo ni uongo kabisa, ni hila za kisiasa na kutaka kuwadhoofisha wadai haki yao ya muungano! msirudi nyuma vijana ! endeleeni kudai haki yenu ni muungano gani mnautaka ! dunia sasa hivi watu wameamka sio mambo yale ya kizamani jamani!

Hamna lolote!!

Kazi ya TISS hii!!!
 
dah ccm kweli mahodari kwa propaganda. jana niliziona zile karatasi zinagaiwa pale kisonge(maskani ya ccm) hao viongozi wa uamsho hakuna hata mmoja mpemba, sheikh mselem ni mdonge(unguja) juma musa aliekamatwa juzi akasababisha fujo mdonge(unguja) azzan mfenesini unguja, faridi mama yake pemba baba yake unguja. sasa sijui muamsho gani wanaosema wao! wanataka wawagawa wazenji ili wawastopishe na harakati za kudai zenji yao.
 
Hivi MPEMBA na M-UNGUJA ntawatofautishaje? Maana Bibi zetu wa huku Bara walibakwa na waarabu
Mm natoa shuume wote wafukuzwe huku bara watu gani wabaguzi wakubwa wanawaita wenzao Punda hapandi Muscat watoke kote Namanga, Kariakoo Bungeni, Wizarani hata na
 
Huu waraka kwa asilimia 100 haujaandikwa na UAMSHO bali umeandikwa na serikali ikishirikiana na ccm ili kuwagawa wanachi wa zanzibar katika jitihada zao za kuupinga muungano. Mimi niko Unguja na hakuna hata mkazi hata mmoja wa unguja anayeupenda muungano wao huu wa kinyonyaji.
 
Hii inanikumbusha maneno ya busara ya baba wa taifa hayati Mwl. J. K. Nyerere. Dhambi ya ubaguzi inaanza kuwatafuna. Walianza kwa kuwabagua wabara na sasa wameanza kubaguana wapemba na waunguja.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…