Waume kazi tunayo

Waume kazi tunayo

Senior Lecturer

Senior Member
Joined
Jan 19, 2013
Posts
177
Reaction score
74
CHONA wa CHILONWA!

Tuliooa tuna kazi kubwa!

Ni hivi, kuna mdada mrembo na ana shule yake ya kutosha kichwani, mke wa mtu, ana kazi yake, kuna magumu anayapitia, nikawa ni miongoni mwa washauri wake (kwa yeye mwenyewe kuja kunitaka ushauri!)

Kutokana na yale magumu anayopitia na zile shauri zangu, kukatokea mawasiliano ya mimi na yeye ya mara kwa mara tofauti na mwanzoni, tukajenga mahusiano ya kawaida sana, mchanganyiko wa aina ya kaka-dada ama urafiki, ambao haukunitisha hata!

Sijui ikawaje, yale mazoea yamekuwa tabu! Sasa bidada analazimisha mahusiano ya kingono na mimi. Wala hakuwa na ugumu wa kuficha, alionyesha hisia na baadae akatamka kabisa. Nimeshindwa kuamini kinachontokea! Kiukweli sina interests nae, na kadri ninavozidisha kumkwepa ndio anazidi kuja! Simfahamu mumewe wala hamfahamu mke wangu! Nakiri kosa la kukubali kumsaidia ktk yale magumu yake, leo nayaona majaribu dunia - mke wa mtu! Hatua nilizochukuwa:
  1. Nimeshamtakia kuwa hatuwezi kuwa wapenzi! Nina ndoa yangu!
  2. Nimekata aina zote za mawasiliano (simpigii, sichat nae)!
  3. Sikubali offer yake yoyote ile!
  4. Nimemueleza hatari za jambo analolitaka, (ndio kwanza kasema sisi ni watu wazima)

Kwa wale tuliooa, nawasihi tuwe karibu na wake zetu, wawe ni zaidi ya marafiki zetu, zaidi ya ndugu, sina ushahidi lkn nahisi huyu bidada ana vitu vidogo vidogo mno, anavikosa kutoka kwa mwenza wake. Bado hakuna dalili ya kumuweka MBALI na mimi! Na ktk vitu nilivomsaidia hakuna hata kimoja interms of cash, ilikuwa ni ushauri tu!
Nipo ktk majuto huku nikitafuta dawa ya kujinasua!
 
Unastahili big up Senior Lecturer... Wanaume mu-wadhaifu sana,hapa tungeambiwa nimeshapiga...wana JF nisaidie jinsi ya kujinasua maana mke wangu anaelekea kujua.. #nimekupenda buree
 
Last edited by a moderator:
Endelea na msimamo wako, sio kwa huyo tu. Na hata akitokea mwingine, isijekuwa huyo hajakuvutia ukaja shawishika kwa mlimbwende mwingine.

Pamoja na yote hongera sana kwa kuonyesha msimamo
 
Ukiwa na shida na hela huipati au huiokoti, asie na shida nayo anaokota.

Binafsi siachi papuchi isipokua tu za mabinti under 18. Hao hata wakiileta wamezianika nazikimbia ila zingine siziachi.
 
Mh..! mbona kama naona manyoya hapa..hivi unavijua vizuri hivi viumbe au unavisikia..!
 
Hahahaaa mi nna F tena ya zero kabisa. Duuuh au ni kabayaaa hako kabinti kenyewe?
 
safi sana, hukuja na hoja hapa ya kulia lia eti unaomba ushauri ufanye nini. ushafanya maamuzi kama mwanaume alaf unatupa taarifa na kutuasa tuwe karibu na wake zetu.
hongera sana kaka. Mungu akutie nguvu ilishinde hilo jaribu.
 
Mh. Nirahisi zaidi kwa simba kugairi kula swala wakati ananjaa kuliko mwamaume kukataa kula papuchi, una roho ya ajabu bro kama kweli lakini. nita kupm kwa mshangao zaidi
 
Duuuh kwa mwanaume rijal ni mtihan mgumu sana anyway kwa vile wadau wengi wameamini
kwamba we ni jembe basi nisiwe mchoyo wa kupa gwaraaaa
 
Duuuh kwa mwanaume rijal ni mtihan mgumu sana anyway kwa vile wadau wengi wameamini
kwamba we ni jembe basi nisiwe mchoyo wa kupa gwaraaaa

Mkuu FANUEL, nashukuru sana, dunia imeshakuwa sio sehemu salama, hakuna wa kutulinda sisi na watoto wetu, tujilinde wenyewe!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom