Watuhumiwa 564 wa madawa ya kulevya wakamatwa kati ya Julai 2015 hadi April 2016 mkoani Mbeya

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,621
8,411
dawa(5).jpg



Zaidi ya kilogramu 730 za dawa za kulevya za aina mbalimbali ikiwemo Bangi,Mirungi na Heroine zimekamtwa katika matukio 409 huku watuhumiwa 564 wakikamatwa katika kipindi cha kuanzia Julai mwaka jana hadi Aprili mwaka huu mkoani Mbeya.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Amos Makalla ameyasema hayo wakati akipokea mwenge wa uhuru ambao umeanza mbio zake mkoani humo ukitokea mkoa wa Iringa.

Akitoa ujumbe wa mwenge kuhusu utumiaji wa dawa za kulevya,kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa,George Jackson Mbijima amesema dawa za kulevya zimekuwa na athari kubwa kwa jamii hasa vijana ambao wanapotumia hupoteza mwelekeo wa maisha yao.

Mwenge wa uhuru ukiwa katika siku yake ya kwanza mkoani Mbeya umekimbizwa katika Halmashauri ya wilaya ya Mbarali ambako umezindua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi tisa yenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni tano.

Chanzo: Capital Radio
 
waende zao uko,sasa hayo madawa mbona hatuyaoni,wanakamata madawa alafu wanayayudisha tena mtaani,shenzi taipu.juzi kati apo apo mbeya wamemfunga jamaa m1 miaka kama30 kwa usafirishaji wa madawa lakini kafungwa wakati kidhibiti halipo ubaoni,jamaa alikamatwa kama 2010,..nyinyi na mbio zenu za mwenge mtuonyeshe vizibiti mnapeleka wapi?especial unga(heroin)sio mnatuonyesha mirungi,damn it.
 
Back
Top Bottom