Traxtion
JF-Expert Member
- Dec 10, 2021
- 5,897
- 11,793
Tokyo Japan
Wengi wetu tunawachukulia Wazungu kama watu wenye ustaarabu lakini sio kweli kama tunavyodhani.
Japan ina watu waliostaarabika kuliko wazungu na kwa mtu yoyote anayeijua Japan anaweza kunielewa.
Osaka, Japan
Wajapan wanazingatia usafi, ukimya, ustaarabu na wengi wao hujali mambo yao hata treni za Japan huwa zipo kimya sana.
Japan hupokea takribani watalii milioni 25 hadi 35 kwa mwaka. Siku hizo watalii wamejaa na kuwa kero Japan huku wengi wao wakiwa ni watalii kutoka nchi za West, yani Nchi za Magharibi (including USA)
Siku za usoni kumekuwa na video nyingi za influencers jinsi walivyokuwa kero Japan kwa tabia zao zisizokubalika Japan
Kwa mfano angalia hii video, huyu dogo kutoka Ujerumani anazunguka nchi mbalimbali na spika yake then anaanza kupiga mziki kwenye mitaa. Kaenda pia kufanya hivi kwenye treni ya Japan ambapo watu wamezoea ukimya. Watu hawamwambii kitu ila kwenye sura zao unaweza kuona wanaboeka hadi mtu mmoja akaamua kuizima spika yake
Siku hizi watu wengi wamekuwa kero huko Japan. Wanaingia wanaanza kucheza mziki kwenye treni, wanapiga picha watu bila ridhaa yao, wanabembea na kufanya utoto kwenye maeneo ya kidini ya Kijapani ambayo Wajapan wanayaheshimu, wanajirekodi wanafanya Yoga kwenye ma temple ya kijapani yanayoheshimiwa na wana act kama vile wako nchini kwao bila kujali utamaduni wa Wajapani
Ukiingia mtandaoni utakuta video nyingi sana kuhusu namna ambavyo watalii wamekuwa kero Japan. Watu wengi wanapenda Japan kupitia utamaduni wao kama vile manga, Anime nk na kila mtu akiangalia Anime anatamani kutembelea Japan. Sio jambo baya lakini ni muhimi kuheshimu tamaduni za watu unapoenda kuwatembelea. Uafrika wako uache huku, ukienda kule ishi Kijapani. Na nina uhakika Waafrika wakifika Japan wanakuwa wastaarabu
Shida ni hawa Westerners, wanajiona kwamba wao ni VIP eti kisa tu wamelipa maelfu ya dollar kwenda Japan kwa hiyo wanajihisi Japan yote ni yao na wanaweza kufanya chochote for the sake of Content creation
Hii video ya mwisho inaonesha baadhi ya watalii wanaojiita Content creators wanavyoleta kero Wajapani
View: https://youtu.be/BR7B0Pjh3lE?si=mlkrcqWN_UH-2x59
Mwisho wa siku, tujifunze kuwa wastaarabu na watulivu kwenye nchi za watu. Sio kila sehemu unafanya unavyojisikia
Japan is not AMERICA. Respect the culture