Watu wasijitoe ufahamu, hakuna mwaka wowote kipindi cha mwendazake Ripoti ya CAG imewahi kuwa nzuri

Opportunity Cost

JF-Expert Member
Dec 10, 2020
9,035
6,907
Kumekuwa na habari nyingi za waganga njaa na wanufaika wa utawala wa mwendazake kwamba eti anachafuliwa Ili kufuta legacy yake.

Binafsi nimekuwa mfuatiliaji wa Ripoti za CAG yangu mwendazake ashike madaraka na hakuna hata siku moja Ripoti iliwahi kuwa nzuri chini ya utawala wake.

Miaka yote kumekuwa na uozo huo huo na mbaya zaidi uozo umekuwa ukiongezeka na hakuna hatua zozote ambazo serikali ya mwendazake ilichukua kubadili mambo.

Tofauti iliyopo sasa ni kwamba CAG ametakiwa kutamka yote sio sawa na kipindi kile ambapo alichagua ya kuongea.

Nadhani mnakumbuka kashfa ya 1.5trilioni na uozo wa fedha za matibabu ya spika na matumizi mabaya ya wizara ya maliasili na taasisi zake kujilipa posho.

Nadhani hata Ripoti ya sasa ni muendelezo wa uozo ule ule wa serikali ya mwendazake na bado CAG amepitia juu juu tuu kwenye masuala ya ndege na miradi mikubwa.

Kwa maana hiyo waimba mapambio na wanufaika wa mwendazake watulie maana waliwaziba watu midomo kwa mkono wa chuma huku wakiimba propaganda ya uzalendo na kutetea wanyonge huku wakijinufaisha wao na genge lao.

Muacheni mama asimamie uhuru wa kujieleza Ili kukomesha tabia za wizi na kuwaumbua wezi.
 
Ripoti ya 2018/19 ilikuwa mbaya vile vile, isipokuwa media hazikupata muda wa kujadili. Nenda kweny udart kweny ripoti za nyuma, kuna almost billion 5 zimepigwa, nenda halmashaur ya chunya mirad mingi ya wiz, nenda kyela. CCM bado ni tatizo!
 
Tunahitaji katiba mpya itakayoimarisha uhuru wa taasisi kama za CAG, DPP na AG. Bila hizi taasisi kufanyika huru itakuwa vigumu sana kuwawajibisha viongozi, hasa mfalme mwenyewe na wale wanaomzunguka.
 
Tunahitaji katiba mpya itakayoimarisha uhuru wa taasisi kama za CAG, DPP na AG. Bila hizi taasisi kufanyika huru itakuwa vigumu sana kuwawajibisha viongozi, hasa mfalme mwenyewe na wale wanaomzunguka.
Lini ilikuwa nzuri, siyo JPM tu. Tangu ma rais wote. Mwinyi, benjamin, JK na sasa JPM. Huu tumejua zaidii kwa sababu mmama wa mipasho na JK wanataka kujaza mashimo. Filling holes
 
Ripoti ya 2018/19 ilikuwa mbaya vile vile, isipokuwa media hazikupata muda wa kujadili. Nenda kweny udart kweny ripoti za nyuma, kuna almost billion 5 zimepigwa, nenda halmashaur ya chunya mirad mingi ya wiz, nenda kyela. CCM bado ni tatizo!
Sio tuu media bali yeyote hakutakiwa kuongelea habari za wizi na ufisadi chini ya mwendazake aliyekuwa anadanaganya umma na kueneza propaganda kwa mtutu
 
Hata mimi nashangaa, kazi CAG ni kuibua madudu au kuna mwaka katika awamu zilizopita ripoti ya CAG iliwahi kuwa nzuri?
Pamoja na hilo ,ishu ya msingi inabakia ni kwa nini ccm na serikali yao huwa hawachukui hatua ya kuzuia wizi na ufisadi? kama wananufaika hivyo watu tuwafyekelee mbali 2025
 
Lini ilikuwa nzuri, siyo JPM tu. Tangu ma rais wote. Mwinyi, benjamin, JK na sasa JPM. Huu tumejua zaidii kwa sababu mmama wa mipasho na JK wanataka kujaza mashimo. Filling holes
Kwa nini alikuwa anatumia nguvu kuficha na kuonesha kile tuu anachotaka kionekane? yupi mzalendo aliyeficha wizi huku anatudanganya au wanaotuonesha kwamba wizi upo tuchukue hatua? JK na Mama wanaingiaje hapa,kwani Kichere kakiuka katiba na kazi yake?
 
Hamna mwaka baada ya 2005 ambapo CAG aliposoma taarifa ikakosa madudu,tena katika Miaka kumi yaani kati ya 2005 hadi 2015 ndo Miaka mibaya zaidi kwani ufisadi ulikithiri na kuwapa ajenda ya ufisadi wapinzani na hata kujiuzuru kwa baadhi ya mawaziri.GAG kwasasa anachofanya ni politics kwa manufaa ya wahalibifu
 
Ripoti ya 2018/19 ilikuwa mbaya vile vile, isipokuwa media hazikupata muda wa kujadili. Nenda kweny udart kweny ripoti za nyuma, kuna almost billion 5 zimepigwa, nenda halmashaur ya chunya mirad mingi ya wiz, nenda kyela. CCM bado ni tatizo!
Media zilishikwa koo
 
Hamna mwaka baada ya 2005 ambapo CAG aliposoma taarifa ikakosa madudu,tena katika Miaka kumi yaani kati ya 2005 hadi 2015 ndo Miaka mibaya zaidi kwani ufisadi ulikithiri na kuwapa ajenda ya ufisadi wapinzani na hata kujiuzuru kwa baadhi ya mawaziri.GAG kwasasa anachofanya ni politics kwa manufaa ya wahalibifu
2016-2020,ufisadi ulitamalaki sana isipokuwa hakukuwa na chombo au nyenzo yoyote ya kuweza kujua ukweli kutokana na kuminywa kwa ukosoaji,uhuru wa vyombo vya habari,taasisi za kiraia nk nk hivyo wapinzani au wananchi hatukujua kinachoendelea.

Katika historia ya nchi hii ni awamu gani uliwahi sikia wizi wa 1.5T? Au matumizi ya pesa ambayo hayakuidhinishwa na serikali? Hizi 3.9T za kutengeneza ndege hewa wewe uliwahi zisikia wapi.

Unajua kwa nini vyombo vya habari vilizuiwa kurusha picha za makazi ya Rais kule Chato kama tulivyoona Kwa marehemu Mkapa na viongozi wengine?
 
Back
Top Bottom