MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,604
Nimeshaisoma Mkuu. Ingawaje ni link ya miaka minne nyuma, bado kuna uwezekano mkubwa wa kuwa baadhi ya magenge hayo na pengine yote yakawa yanafanyakazi.MAMMAMIA hiyo linki aliyoiweka Mzalendo452 inafaa kusomwa (kama haujaisoma).
Pamoja na hayo, tusisahau kuwa kwa nyakati za sasa hata mtu binafsi ni rahisi kupata silaha, hasa Kenya kutokana kwanza na hiyo historia ya magenge ya vurugu lakini pia kupakana kwake na Somalia. Na hawa watu binafsi ndio hatari zaidi kwani wanaweza kujichanganya popote bila ya kutiliwa shaka.
Sababu za mtu/watu binafsi zinaweza kuwa nyingi, ikiwemo kulipiza kisasi (japokuwa aliyekuudhi ni mtu mmoja na kutojali utaua wangapi). Tuone yanayotokea nchi za wenzetu ambako kwa mfano, mwanafunzi akifeli mtihani tu anaweza kuingia darasani na kuua umati; ukiwachia personal frustrations due to life hardships.
Ninawapa pole sana Wakenya, lakini kwa Tanzania (ambako tunaimbishana wimbo wa maliwazo ya KISIWA CHA AMANI) ningependa kuonya Halahala mti na macho.