Watu pori - Nafsi ya mtu

Watu pori - Nafsi ya mtu

NGAYANIMO

Member
Joined
Feb 17, 2026
Posts
36
Reaction score
55
NAFSI YA MTU.

Watu pori a.k.a washamba a.k.a washamba a.k.a washamba /nyani wapya msitu wa zamani beat mjerumani mambo yote kwa Bonnie/

Verse ..1 ( mc koba)

Sikiliza haya ninayo kueleza leo na kesho usije kuyapuuza / kwenye mizizi ya Dhambi wivu ndio Unaongoza / kwa upande wa Mema upendo ndio wa kwanza/

Tena kabla ya kutenda nakuomba ufikiri kwanza/ kwani ukienda papara utakuja kuteleza / na kuaza kui laumu nafsi baada ya kuumiza / na ukaja kufeli ulilopanga kutimiza/ kama Sanaa ni Sanaa " ni Sanaa" we fanya kweli sasa wacha kushangaa/ kama uja kubalika usianze kuleta visa uzindi kuwajibika/ na uachake kabisa..!! We pana kushoto usiloliweza lione ka Gari la moto/ Mc kaa tayari kupokea changamoto/ ni Mc koba napenda mabadiriko/ Daruni nishatazama 🎤 mic kasema "sio lazima wote tuimbe" shtuka wacha uzembe/ mkulima shika jembe..!! / ulimwengu wa leo mi nakushangaa unaongopa "ukwimwi" huku una angaika Aaah/ ..

Unachekesha una amini Wazungu wakati Mungu unakataa Eeeh / Ewe mwana Elimu shika pen ujinga Sumu / uliza waliochezea hiyo nafasi ya muhimu / walichokipata nini..? Zaidi ya kusota na kuzuga mitaani Eeeh/...

Chorus ( mc koba)

Sogea karibu nikuambie Eeeh/
Nitakayonena uyasikie Eeeh/
Watu wananishangaza mie Eeh/
Nafsi zao hasieleweki eeeh/
Mkanye mjinga akuchukie Eeh/
Mipango yako hakuharibie Eeh/
Na sauti inanichosha mie Eeeh/

Eeeh eeeh eeh...!!

Verse 2..( Dogo ditto)

Inanichanganya kuona mnyonge anatukanwa / hata kile kidogo alicho nacho ana nyang'anywa..Aah..!! / ni nafsi ya mtu kwa vile imekosa Imani / basi ni chuki moyoni kila siku hakuna Amani " hakuna amani"/ namshangaa....! moyoni ana furaha kwenye Bar / Mambo yaki haribika kwenye ibada ana haha " ana haha./ ni mtu mzima ukimuona utamuita Babu/ anaona Aibu nyumbani ni Tabu tu / maisha yake ni kama adhabu akienda Bar miguu juu / mbona ana jenga chuki sababu yule kapata/ wakati sehemu ya ibada ana kesi kaiba sadaka/ si unge fanya kazi ujitume brother unge zinyaka .... si ungefanya kazi ujitume uenda ungezipata / ni siku gani..? Muda gani..? Na nchi gani..? Wamekuambia uangushwa kama majani/ kifkra upo hoi bini Taabani bila kutafuta uzipate kakuambia nani..?/ fanya kazi ...........usinichekeshe unapenda ....!! staff uta ombaje kazi mchori wakati unaongopa wafu..

Chorus ( mc koba)

Sogea karibu nikuambie Eeeh/
Nitakayonena uyasikie Eeeh/
Watu wananishangaza mie Eeh/
Nafsi zao hasieleweki eeeh/
Mkanye mjinga akuchukie Eeh/
Mipango yako hakuharibie Eeh/
Na sauti inanichosha mie Eeeh/

Verse..3 ( mc koba & ballet)

Ni nafsi ya mtu imekosa Imani/iwe dunia na hata mbinguni/ binadamu wa leo afadhiliki/ mpe kila kitu mpe atakushiti..

Maana wema unapozidi mauti/
Wana lengana kwa bunduki na manati/
Wana rongana kwa uchawi wa saniki nafsi zao zimejaa chuki binafsi/..

Verse..4 ( afande sele)

Mwingine...Mwingine...siku nyingine....mtu mwingine....
Anakuja kwako anashida ameshindwa Tena mikono Nyuma / amekonda "amekonda" una mtazama kwa huruma na kukwepa lawama/ unasema loooh..!! Lazima nimpige Tafu kwa moyo mkuchufu/ tena bila kujali skendo zake za uharifu / na uchafu wa mwili na Tabia unakua nae unaishi nae kama wife for life kumbe ni knife 🔪/ ana kusifu machoni moyoni ana kusanifu/ ana beef Aiseeh...!! ni mbwa mwitu anae winda kuliko chatu/ ndio nafsi yake / hata U mpe kila kitu sasa basi/ kama wasipo rudi wanao kwenda mbele za haki / ndivyo kilicho pinda kime pinda akinyoosheki/ basi nawaambia naku Abia asie shiba kwenye sinia/ hato shiba kwenye kijiko/ na tena nawaambia utafundishwa na Dunia kama ujafunzwa na mama Yako/ shauri yako Simba mzee....

Chorus..( Mc koba)

Sogea karibu nikuambie Eeeh../
Nitakayo nena uyasikie Eeeh./
Watu wana nishangaza mie Eeeh./
Nafsi zao hasielewiki Eeeh./
Mkanye mjinga akuchukie Eeeh./
Mipango yako hakuharibie Eeeh/
Na sauti inanichosha mie Eeeh /

Eeeh Eeeh Eeeh ..

Ukwaju wa kitambo
0767 542 202
1771961556290.jpg
 
  • Thanks
Reactions: K11
Kipindi hicho tulikuwa tunasikiliza nyimbo za wasanii wetu bila kificho kwa vile waliimba na kuzungumzia mambo positively.

Leo hii kusikiliza nyimbo za akina Harmonize sijui Zuchu zimejaa matusi, unajificha mithili ya mtu anayesikiliza au kutazama kazi za "Rachel Dangwa".
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom