Watu huona nini wanapokaribia kufa?

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
361,100
Reaction score
831,745
Niandikapo mistari hii kuna watu wanakufa wengine watakufa baadae wengine usiku mwingi dunia ikiwa tulivu wengine kesho na kuendelea...mbele yao nyuma yetu

Kitu cha kushangaza kutoka wale walionusurika kifo ni simulizi zao za yale waliyoyaona au kukutana nayo pale roho zilipokuwa katikati ya kuzimu na dunia.

Lakini pia habari nyingine zinasema kuwa watu wanapokuwa katika kipindi hicho,wengi
- huona maisha yao yakipita mbele ya macho yao kama sinema
-wengine mabaya yao hujifunua na kuyasimulia bila kujua
-wengine huomba msamaha
-wengine huomba msaada
-wengine hujiona wakienda mbali sana
Wengine huona moto, malaika au viumbe wa ajabu
Kwa ujumla wake hali hii huelezewa kama hari za kifo...ni kipindi kigumu mno kwa wale wanaokutana na hizi mambo.

Lakini kuna wengine hufa wakiwa usingizini kwa amani kabisa wala bila kujitambua kuwa wamekufa , hawa nyuso zao huonekana zimetulia kabisa ni kama wamelala.

Kitu cha ajabu ni wale wafao huku hari za kifo zikiwaandama nyuso hukunjamana na kubaki na maumivu hata baada ya roho kuachana na mwili.

Usiwe mtu wa vinyongo Usiwe mtu wa dhuluma Usiwe mtu wa visasi Usiwe mtu wa rohombaya, vitu hivi huzalisha roho zitakazokutesa mpaka kifo....kama una nyongo umezihifadhi tumboni jitahidi kuzitapika usiku huu..ya kesho huyajui
 
Huu ni ulimwengi mwingine, uelewano kati ya Roho na Nafsi. (Wachache wataelewa ) ushirika wake hufanya neema kuonekana katika mwili, wengi husema kubarikiwa, mvutano wake hufanya uzito hata kwa mambo mepesi.
 
Bwana mshana jr kuna uzi umeandika kuwa kifo ni hatua ya kuingia maisha mengine bora, sasa mbona unachanganya hapa tena mauza uza haya?
 
Bwana mshana jr kuna uzi umeandika kuwa kifo ni hatua ya kuingia maisha mengine bora, sasa mbona unachanganya hapa tena mauza uza haya?
Ni kweli unaitwa sanaa ya kifo..ule ni baada ya kujiandaa kwa mtihani wa kifo na baadae kuingia huko kifoni
Hapa ni zile sekunde au dakika za mwisho between life n death or near to death experience
Kwa muktadha wa post ile yaani kile kimuhe muhe cha mtihani wa kifo
 
Je ulishawahi kufa?
 

Hadi najuta kuisoma hii sredi yako, timing yake sio kabisa, tunatishana mkuu,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…