Watu 8 wafariki ajalini Mbeya

Itv wanatangaza hivi sasa. Coaster imegongana na prado huko Mbozi, ilikuwa inatoka Tunduma kwenda Mbeya. Watu 8 wamekufa na majeruhi ni zaidi ya 20. Chanzo mwendo kasi.
 
RIP bandugu.
hivi huu mwendo kasi hadi lini? Madereva huwa wanavuta bange au tatizo ni nini jamani.
 
Coaster ya iitwayo mbombo imegongana na prado na kusababisha vifo kadhaa n majeruhi!idadi kamil ya waliopoteza maisha bdo haijafahamika!
Source:itv
 
Ajali mbaya imetokea baada ya Coaster ya abiria iliyokuwa inaelekea Mbeya kugongana uso kwa uso na prado.Ajali imetokea kati ya Tunduma na Mbeya mjini.Watu 8 wamekufa zaid ya 20 wamejeruhiwa.TUNAKWISHA JAMANI
 
Leo jion imeripotiwa kutokea ajali mbeya katika eneo la mbozi,likihusisha gari aina ya coster toka Tunduma kuelekea mbeya mjini imegongana na gari aina ya prado na watu nane kufariki papo hapo..jamani tuiombee Mbeya
 
huko mbeya kuna nini?si ndio mkoa unaosemekana kuwa na makanisa mengi kuliko yote hapa nchini?kweli mpinga kristo yupo kazini
 
Coaster ya iitwayo mbombo imegongana na prado na kusababisha vifo kadhaa n majeruhi!idadi kamil ya waliopoteza maisha bdo haijafahamika!
Source:itv

Inaniacha hoi sana kwani kumbukumbu zangu zinaonyesha kuwa ktk eneo hilo hilo mwezi wa kwanza mwaka huu gari nyingine (mbombo trans ilichomwa moto na wananchi WENYE HASIRA KALI baada ya kugonga na kuua kutokana na mwendo kasi. SIJUI HIZI NDIZO FEDHA ZA MIKATABA??????????????????
 
mkuu asante kwaku2fikishi taarifa hii, ROHO ZA MAREHEMU WOTE WALIO AGADUNIA KTK AJALI HII ZIPATE REHEMA KWA MUNGU ZIPUMZIKE KWA AMANI AMEN, ee mungu uwa ponye majeruhi wote walio nusurika ktk ajali hiyo uwa jalie moyo wa imani madaktari wote wanao wapa huduma Amen, ee baba zifariji familia za wote walio poteza uhai Baba umetoa baba umetwaa,
 
Tatizo la ajali si mwendo kasi tu, uwezo mdogo wa madereva wengi na pia forged driving licences pamoja na ufundishwaji duni! Nimewahi shuhudia makutano ya barabara ya Mwenge mwanafunzi kwenye gari la Victoria driving school akiwa na mkufunzi wake akivuka taa nyekundu bila wasiwasi ilhali madereva wengine wakiwa wamesimama, unategemea nini mtu kama huyo akipewa usukani wa basi?
Utawala wa sheria ni muhimu sana jamani, hebu fikiria jamii nayo inasema ukiendesha kwa kufuata sheria utagongwa! Jamani tunahalalisha wenyewe maasi halafu tukija kusikia watu wamekufa kwenye ajali tunabaki kusema mwendo kasi!
Barabara nyingi ni finyu ila ukiwa dereva makini bado utafika salama.

Poleni wafiwa.
 
Kweli yataka Moyo coz matukio mengi ya mwaka huu, Mbeya inatafuta kushika namba moja. Na kama kusingekuwa tena na hz hekaheka za uchaguzi huko Igunga nadhani habari nyingi zingelikuwa za huko Mbeya. R.I.P wale wote waliofariki na Mungu awajaalie wale wote waliojeruhiwa wapone haraka.
 
Tatizo la ajali si mwendo kasi tu, uwezo mdogo wa madereva wengi na pia forged driving licences pamoja na ufundishwaji duni! Nimewahi shuhudia makutano ya barabara ya Mwenge mwanafunzi kwenye gari la Victoria driving school akiwa na mkufunzi wake akivuka taa nyekundu bila wasiwasi ilhali madereva wengine wakiwa wamesimama, unategemea nini mtu kama huyo akipewa usukani wa basi?
Utawala wa sheria ni muhimu sana jamani, hebu fikiria jamii nayo inasema ukiendesha kwa kufuata sheria utagongwa! Jamani tunahalalisha wenyewe maasi halafu tukija kusikia watu wamekufa kwenye ajali tunabaki kusema mwendo kasi!
Barabara nyingi ni finyu ila ukiwa dereva makini bado utafika salama.

Poleni wafiwa.
Kweli kabisa uliyosema.
 
sishangai mbeya kuna pahali tuliwahi kaa zambia road nzovwe basi kila mvua ikinyesha tulikua tunasogea jirani na barabara kuangalia sarakasi za magari na majeruhi wanavyokufa
its very bad memory i have in my head always
 
Back
Top Bottom