Watoto wa miaka mitatu boarding Tanzania

Watoto wa miaka mitatu boarding Tanzania

Naamini wengi waliocoment hapa siyo wazazi,
ili kuweza kumtunza huyo mtoto mzaziinahitajika afanye bidii katika kazi yake,
vipi kama kazi zinamfanya ashindwe kuwa na mtoto kwa muda mrefu?
Atamwachia msichana wa kazi?
Wasichana wenyewe ndo hawa!!
Kwangu heri aende huko boarding kuliko nimuweke mtoto kwa ndugu ama kumwacha na msichana wa kazi.

....si sababu!
"kumbuka kulea mimba si kazi' kazi ni kulea mwana".

...mnao wapelekea wawalelee, hawajui kulea! Na watoto walio wengi mnao wapeleka kwenye hizo shule wanakuwa bado kujitambua:
"Matron wenyewe 'walio wengi' hawajawahi kuwa na mtoto! kazi ni kuelekeza watoto wakubwa kutawaza wadogo zao, wao kwa wao"
 
Mara nyingi utakuta wazazi wa watoto wa namna hii walipata hawa watoto kama matokeo ya kujifurahisha katika tendo la kujamiiana, sio kama matokeo ya kuwa na nia ya furaha ya kuwa na watoto. Kwao kuzaa si tokeo la kupangwa.

Hakuna kipindi watoto wanakuwa so sweet kama umri wa miaka 2-4. Sasa ni mtu ambaye haoni hilo anaweza kuamua kutenganishwa na watoto katika kipindi hicho na kukikosa. Mzazi wa namna hiyo ana matatizo ya kisaikolojia.
 
Kati ya mambo yanawafanya watoto wawe na tabia ambazo hazistahili katika jamii ni wazazi kutokuwa na muda na mwanae, mtoto anakuwa na tabia za ajabu ajabu baadae unaishia kulalama mtoto hakuheshimu.

Binafsi Siungi mkono kabisa swala la mtoto kupelekwa boarding school katika umri mdogo kiasi hicho walau akimaliza darasa la saba anakuwa amesha jitambua ndio unaweza mpeleka boarding.

Yupo mtoto wa jirani yangu miaka 5 wa kiume walimpeleka boarding school hapa Dar yenye watoto kuanzia nursery mpk std 7 , baadae amerudi likizo mtoto haeleweki kumbe wenzake wakubwa wameshamchezea nyuma.

Akaja kwangu kuomba ushauri na eti tumuombee mwanae nikamwambia kwamba hayo ndio matunda ya mzazi asiyetaka kutekeleza wajibu wake.. nikamwambia uamuzi ni wako badili mtizamo wako mtoto atabadilika au endelea na mtizamo wako ule matunda yake.

Kweli amemuhamisha shule yuko day care sasa.. ila ndio hivyo tena seal broken..
 
Halafu watoto wakiwa shababi na mabazazi mnaanza kushikana uchawi.
 
Ki ukweli mtoto akiwa mdogo anastahili kujifunza tabia za familia yake na sio tabia ya familia nyingine. Mtoto atakua na tabia ambazo anazipenda matroni lakini sio wewe mzazi sasa ni bora huyo matroni awe mwenye tabia nzuri, kama tabia yake ni mbaya UTAJUTA.

Si sahii mzazi kusema eti hana muda wa kukaa na mtoto eti yuko bize na kazi. Kumbuka kazi itaisha na utabaki na mtoto wako ambaye hana mapenzi na wewe kabisa na mwenye tabia ambazo wewe huzipendi na hawezi kukaa na mtu yeyote zaidi ya getto na wenzie kwani kazoea kuishi kimakundi toka akiwa mtoto.

Mtoto anaanza kujifunza akiwa na miaka 2,3 sasa wewe ndo unamtupia mwenzio, lazima utakua na mtindio wa Ubongo na Taahira ya akili, poleni saana mnaaoona ubora kuwapeleka watoto boarding ili muwe free
 
Naamini wengi waliocoment hapa siyo wazazi,
ili kuweza kumtunza huyo mtoto mzaziinahitajika afanye bidii katika kazi yake,
vipi kama kazi zinamfanya ashindwe kuwa na mtoto kwa muda mrefu?
Atamwachia msichana wa kazi?
Wasichana wenyewe ndo hawa!!
Kwangu heri aende huko boarding kuliko nimuweke mtoto kwa ndugu ama kumwacha na msichana wa kazi.
kwan daycare hazipo mkuu?,mpeleke mwanao daycare then jioni mpitie..
 
Naamini wengi waliocoment hapa siyo wazazi,
ili kuweza kumtunza huyo mtoto mzaziinahitajika afanye bidii katika kazi yake, vipi kama kazi zinamfanya ashindwe kuwa na mtoto kwa muda mrefu?

Atamwachia msichana wa kazi?
Wasichana wenyewe ndo hawa!!
Kwangu heri aende huko boarding kuliko nimuweke mtoto kwa ndugu ama kumwacha na msichana wa kazi.

You are not serious!! Hapa hatuzungumzii kuwa na mtoto 24 hours 7 days a week!Hata kama unaonana na mwanao kwa masaa 3 tu INATOSHA SANA!Kwanza sijui wazazi wengine wana akili za namna gani, yaani wewe mama kweli mtoto wako wa miaka 3 unampeleka Dodoma wewe uko Mwanza for 4 or 3 months?Hivi unapata usingizi kweli?? Mtoto wa miaka 3 kwanza bado anatakiwa kulala na mama yake!!

Anyway, kwa kuwa siku hizi tunashindana kuoneshana nani ana hela sawa tu, wapeleke wanao boarding ila baadae ukija kukuta mwanao wa kiume ni SHOST ndo utatia akili
 
Back
Top Bottom