Muuza simu used
JF-Expert Member
- Aug 23, 2017
- 4,393
- 7,031
Ngoja niende kwenye mada moja kwa moja!ni hivi katika swala la kulea mtoto wako hasa inapotokea mliachana na mama wa mtoto kwa namna moja au nyingine ni changamoto kubwa sana!hasa masingle mother walio wengi wanakuwa na ile hali ya kumkomoa baba wa mtoto kwa namna moja ama nyingine!mfano unaweza ukawa unamuhudumia mtoto kwa kutoa pesa za matumizi lakini pesa haziendi kwenye matumizi husika zaidi ya mwanamke kula good time mjini na hali ya mtoto kuonekana duni kama baba yake hajiwezi,pili either pesa za matumizi ya mtoto anaenda kununuliwa nguo mwanaume suruali flani hivi ili na yeye aonekana amepata handsame zaidi yako!na hali hii huchochea hasira kwa baba wa watoto wengi na kujikuta amesusa hadi kutoa matumizi yenyewe!Tatu pia imekuwa na swala la kawaida kwa masingle mother kutotaka baba wa mtoto asimuone mtoto wake ili mradi tu amkomoe!na kitu kingine asilimia kubwa ya wanawake (single mother)ndio wanaongoza kwa kujaza sumu watoto kwa kumdanganya mtoto mabaya ya baba yake!kuna kipindi wanaenda mbali zaidi hadi kudiriki kwa kumwambia mtoto baba yake amekufa!
N;B,Wanawake tofautisheni kati ya mapenzi na future ya mtoto!mtapata tabu saaana
N;B,Wanawake tofautisheni kati ya mapenzi na future ya mtoto!mtapata tabu saaana