Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,125
Watoto 300 walio chini ya miaka mitano nchini hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na ukosefu wa lishe na asilimia 42 chini ya umri huo hudumaa kutokana na tatizo hilo, ripoti ya shirika lisilo la kiserikali la Save the Chidren imebainisha.
Kutokana na hali hiyo Profesa Joyce Kinabo toka Chuo Kikuu cha Sokoine (Sua) aliye kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa ripoti hiyo jijini Dar es Salaam jana, aliiasa jamii kujielimisha na kuanza kutumia vyakula vya asili vyenye lishe vinavyopatikana nchini ili kupunguza tatizo hilo.
Profesa Kinabo alisema katika uzinduzi uliowashirikisha watoto kutoka katika wilaya za Kinondoni na Temeke, jamii ya kitanzania inaweza ikaliondoa tatizo hilo kwa kutumia vyakula vyenye lishe kwa kila mlo visivyokuwa vya gharama na vinavyokidhi viwango vya Dola moja kwa mlo, vilivyowekwa na Umoja wa Mataifa.
Mmoja wa watoto walioshiriki katika uzinduzi huo, ambaye pia ni Mwenyekiti Msaidizi wa Baraza la Watoto manispaa ya Temeke, Wastara Athumani, aliitaka serikali itenge fedha za kutosha mijini na vijijini kwa ajili ya kuhudumia bajeti ya vyakula mashuleni ili
kuwawezesha wanafunzi kufanya vizuri katika masomo.
CHANZO: NIPASHE
Kutokana na hali hiyo Profesa Joyce Kinabo toka Chuo Kikuu cha Sokoine (Sua) aliye kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa ripoti hiyo jijini Dar es Salaam jana, aliiasa jamii kujielimisha na kuanza kutumia vyakula vya asili vyenye lishe vinavyopatikana nchini ili kupunguza tatizo hilo.
Profesa Kinabo alisema katika uzinduzi uliowashirikisha watoto kutoka katika wilaya za Kinondoni na Temeke, jamii ya kitanzania inaweza ikaliondoa tatizo hilo kwa kutumia vyakula vyenye lishe kwa kila mlo visivyokuwa vya gharama na vinavyokidhi viwango vya Dola moja kwa mlo, vilivyowekwa na Umoja wa Mataifa.
Mmoja wa watoto walioshiriki katika uzinduzi huo, ambaye pia ni Mwenyekiti Msaidizi wa Baraza la Watoto manispaa ya Temeke, Wastara Athumani, aliitaka serikali itenge fedha za kutosha mijini na vijijini kwa ajili ya kuhudumia bajeti ya vyakula mashuleni ili
kuwawezesha wanafunzi kufanya vizuri katika masomo.
CHANZO: NIPASHE