Watendaji wa Mwauwasa: Jiuzuluni!

Watendaji wa Mwauwasa: Jiuzuluni!

tausi2020

Member
Joined
Jul 5, 2025
Posts
67
Reaction score
92
Kwa takribani wiki nzima wakazi wa Nyegezi, Mwanza wamelazimika kuchota maji mitaroni baada ya huduma ya maji kukosekana kabisa bila taarifa yoyote kutolewa.

Cha kushangaza, ni baada ya malalamiko ya wananchi kuibuka ndipo Mwauwasa walitoa tangazo kupitia akaunti yao ya mitandao ya kijamii, wakidai kuwa kuna matengenezo yanayoendelea kwenye chanzo cha maji ambacho Mheshimiwa Rais alizindua miezi michache tu
Hali hii inaleta maswali makubwa:
IMG_2038.jpeg

  • Je, mitambo mipya hii tayari imeharibika au ilikuwa chakavu tangu mwanzo?
  • Kwa nini wananchi hawapewi taarifa mapema bali wanateseka kwa siku nyingi?
Wananchi wanalipa kodi na wanastahili huduma bora. Hii ni dharau kubwa na ishara ya uzembe wa kiutendaji.Mwauwasa imekuwa ikilalamikiwa mara nyingi na sasa tatizo limeonekana kuwa sugu.
IMG_2038.jpeg


Kwa sababu hiyo, watendaji wa Mwauwasa mnapaswa kujiuzulu mara moja.
 

Attachments

  • IMG_2045.jpeg
    IMG_2045.jpeg
    220.7 KB · Views: 15
  • IMG_2044.jpeg
    IMG_2044.jpeg
    253.5 KB · Views: 10
  • IMG_2043.jpeg
    IMG_2043.jpeg
    256 KB · Views: 9
  • IMG_2042.jpeg
    IMG_2042.jpeg
    219.9 KB · Views: 13
  • IMG_2041.jpeg
    IMG_2041.jpeg
    305.4 KB · Views: 11
  • IMG_2040.jpeg
    IMG_2040.jpeg
    352.2 KB · Views: 12
Kanda ya ziwa kuna shida ya maji. Kuna degrees zipo maofisini,mwisho wa mwezi wanalipwa mshahara.
 
Mwauwasa ni jipu. Yaani mara 1000 ya tanesco pamoja na changamoto zote wanajitahidi.
 
Back
Top Bottom