Watanzania wengi hawali balance diet wanakula diet of the balanced budget

mwanazuoni mgeni

JF-Expert Member
Sep 11, 2016
1,944
1,712
Habari wana JF,

Katika jamii nyingi tunazoishi maisha ya watanzania wengi ni level ya kati na ya chini na pia asilimia kubwa ya watanzania hawana elimu ya kutosha kuhusiana na maswala ya afya hivyo basi inapelekea familia nyingi kula chakula kulingana na hela iliyopo na chakushangaza zaidi unakuta kuna aina flani ya mlo ndo unatumika Mara kwa Mara.

Lakini pia ukiangalia upande wa pili hili linasababishwa na umasikini na ukosevu wa elimu kuhusiana na maswala ya afya watu wengi hawajui mlo kamili ni mchanganyiko wa vyakula gani, ninachokiamini ni kwamba hata mtanzania awe wa hali ya chini akiamua kujipangia vizuri mpangilio wa vyakula ataweza, tatizo kubwa ni elimu ya kula mlo kamili watu wengi hawana.

Nimalizie kwa kusema: Kuwa na afya njema inahusiana sana na mfumo wa maisha kwa ujumla pamoja na mlo kamili.
 
Iko hivi unapozungumzia mlo kamili ..ni ule ulio na mchanganyiko wa vyakula vyote muhimu ...yani
Protini hapa kuna nyama,samaki, dagaa, maharage,maziwa ,mayai n.k
Vitamin hapa kuna mboga mboga za majani na matunda
Wanga hapa kuna mahindi, mchele, ndizi, viazi ,mihogo, magimbi.,ngano
Bila kusahau maji safi na salama
Ukijitahidi kwenye kila mlo wako kukawa na mchanganyiko wa vyakula vya kila kundi nililolitaja hapo bhas ujue utakua katika afya nzuri
NOTE: sio kwamba vyote nlivyo orodhesha ndo uvile vyote kwa mpigo hapana yani unaweza ukachukua kimoja kimoja kwenye kila kundi na ukawa umekamilisha diet yako
 
Back
Top Bottom