eistein huyo huyo huyo alisema wajinga huwaona werevu kuwa wajinga na wao wajinga kujiona wao ndio werevu. sasa katika hali hiyo nani wa kumtoa mwingine kule aliko kusiko faa na kumpeleka kunakofaa ni shida maana kila mmoja anjiona yuko sahihi.
yawezekana ukawa na mtizamo wako unauona ni sahihi na wengine wanaona mtizamo wako si sahihi je ni nani mjinga na ni nani anayejua? maana ili jamii isonge mbele inahitaji kufuata njia sahihi na pande zote mbili zinajiona ziko sahihi?
kwa mtizamo wangu binafsi ninaamini elimu ya bure ni ujinga unaotupeleka kwenye umasikini kwa hoja kuwa.
hakuna kitu chochote cha bure, ama tukigharamikie kwa kutumia fedha za pamoja tunazozichanga kwenda kwenye mfuko wetu kama watanzania unaosimamiwa na serikali au tulipie kwa fedha zetu za mifukoni.
fedha tunazochangia kupitia kodi na rasilimali nyingine zinatakiwa kutumika kujenga miundo mbinu kama shule, zahanati, barabara, miundombinu ya maji, umeme, gharama za uendeshaji na utoaji wa huduma kwa maana ya kuwalipa watumishi na kujenga miradi kadha wa kadha ya maendeleo katika jamii yetu.
sisi kama jamii masikini michango yetu ni kidogo sana na hii imepelekea kutuongezea umasikini kwa maana huduma ni duni, bado hali ya miundombinu au facilities za kutolea huduma na utaalamu ni duni na hii imesababisha jamii yetu kukosa huduma.
mtu yeyote anayewaza huduma za bure amepitwa na wakati kwa mtizamo wangu kwa maana hiyo ilikuwa ni mahitaji ya watanzania miaka ya 60 na sabini kutokana na hali ya kimaisha ya watanzania. enzi hizo shughuli za kufanya zilikuwepo lakini watanzania walikosa maarifa. mtu alikuwa anahitimu kidato cha nne anapangiwa kituo cha kufanyia kazi maana watu wenye elimu walikuwa wachache. michango ya jamii wakati huo ilikuwa sahihi kusomesha wanajamii hawa ambao uchumi wao ulikuwa duni hawakuwa na uwezo wa kumudu gharama za masomo.
leo hii uchumi wa watanzania umebadilika na mazingira yamebadilika, watanzania uchumi wao kwa sasa wanamudu gharama za masomo ila changamoto zimebadilika kuwa wasomi wanaanza kuwa wengi kuliko nafasi za ajira, ubora na wingi wa huduma mbalimbali katika jamii ndio imegeuka kuwa changamoto kubwa. watanzania wanaohitaji ajira wamekuwa wengi kuliko nafasi za ajira zilizopo. kwa mazingira haya kwangu mimi naamini ni ujinga kudhani huduma za bure zitakomboa jamii hii.
huduma za bure zitapunguza kiasi cha fedha katika mfuko wetu wa pamoja kinachoweza kutengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo. kupungua kwa uwezo wakifedha na kasi ya kutekeleza miradi ya maendeleo kutapunguza uwezo wetu wa kutengeneza nafasi za ajira mpya hivyo un employment itaongezeka.
hivyo watanzania wa leo wanahitaji fedha zao zinawatengenezee mazingira ya kuzalisha au kupata ajira. hatuhitaji wakulima wetu wawe na digrii kila mmoja ndio tuzalishe chakula cha kututosha na kupeleka ziada nje, tusidhani kukosa elimu kwa watanzania ndio kunasabisha asilimia kubwa ya bidhaa ndogo ndogo kutoka nje.
anayefikiria huduma za bure ni kipofu anayestahili kuongozwa na sio yeye kukaa mbele kuongoza wengine. labda nikuulize wewe mwenyewe unachokitaka maishani mwako ni kitu gani, fedha kidogo ya serikali itumike kukutengenezea mazingira ya wewe kufanya kazi na kuongeza kipato chako au fedha hiyo itumike kusomesha watoto wako katika shule za sasa za serikali na kutoa huduma za afya kwenye vituo na zahanati za serikali bure. kumbuka anayekuambia kuwa atakufanyia yote ni mwongo kwa maana fedha yetu ni kidogo hivyo kiongozi anaweza kufanya moja na sio kwa ubora au kasi unayohitaji bali kwa kasi ndogo.
Albert Einstein alisema "uendawazimu ni kufanya jambo lile lile' mara nyingine na kwa namna ile ile huku ukitegemea matokeo tofauti" pongezi ziwaendee wakazi wote wa mijini isipokuwa mwanza tu wamefanya kazi nzuri. watu wa vijijini wanastahili hayo maisha milele zote