Tukundane
JF-Expert Member
- Apr 17, 2012
- 12,231
- 9,552
Watanzania tumempa kazi Lowassa ya kuichapa CCM,hakuna mtu mwingine anayeweza akawachapa CCM zaidi ya Lowassa kwa kuwa amekaa nao muda mrefu,amefanya kazi katika serekali ya CCM kwa kipindi kirefu,ujanja wao wote na hila zao zote mpaka rangi za nguo zao za ndani ana zifahamu.
Pamoja na propaganda zote zinazopigwa na CCM kuwa Lowassa ni mgonjwa hataweza kuongoza nchi lakini kwa kuwa Lowassa ana wamudu CCM wananchi tutakwenda na Lowassa kwa kuwa kazi ya kuongoza nchi ni rahisi kuliko kazi ya kuwaondoa CCM madarakani kwa kuwa nchi haitegemei kuongozwa na mtu mmoja.
Ugumu wa kazi ya kuiondoa CCM madarakani ulianza kujidhihirisha pale ambapo watu wengi kama Mrema na wengine walipojaribu kuiondoa CCM madarakani wakashindwa kwa kuwa kazi ya kuiondoa CCM ni ngumu kuliko kazi ya kuongoza nchi.Ambayo hata kama utakuwa na nguvu kama tembo CCM inaweza ikakushinda,hata kama utakua na afya iliyothibitishwa na Mungu mwenyewe,kuwa ni mzima CCM inaweza ikakushinda.
Hata kama CCM watapiga propaganda vipi,kuwa Lowassa ni fisadi na kwa kuwa CCM wameshindwa kutuhakikishia kuwa baada ya Lowassa kujiuzuru ufisadi ndani ya serekali ya CCM umekwisha,wananchi tutakuwa na Lowassa.
Hata kama ikitokea Lowassa akafa siku moja baada ya kuiondoa CCM madarakani,watanzania tutamuenzi kama shujaa pekee aliyefanya kazi nzito ya kuiangusha CCM iliyowashinda watu wanaojiona kuwa wana afya bora kuliko wenzao.
Pamoja na propaganda zote zinazopigwa na CCM kuwa Lowassa ni mgonjwa hataweza kuongoza nchi lakini kwa kuwa Lowassa ana wamudu CCM wananchi tutakwenda na Lowassa kwa kuwa kazi ya kuongoza nchi ni rahisi kuliko kazi ya kuwaondoa CCM madarakani kwa kuwa nchi haitegemei kuongozwa na mtu mmoja.
Ugumu wa kazi ya kuiondoa CCM madarakani ulianza kujidhihirisha pale ambapo watu wengi kama Mrema na wengine walipojaribu kuiondoa CCM madarakani wakashindwa kwa kuwa kazi ya kuiondoa CCM ni ngumu kuliko kazi ya kuongoza nchi.Ambayo hata kama utakuwa na nguvu kama tembo CCM inaweza ikakushinda,hata kama utakua na afya iliyothibitishwa na Mungu mwenyewe,kuwa ni mzima CCM inaweza ikakushinda.
Hata kama CCM watapiga propaganda vipi,kuwa Lowassa ni fisadi na kwa kuwa CCM wameshindwa kutuhakikishia kuwa baada ya Lowassa kujiuzuru ufisadi ndani ya serekali ya CCM umekwisha,wananchi tutakuwa na Lowassa.
Hata kama ikitokea Lowassa akafa siku moja baada ya kuiondoa CCM madarakani,watanzania tutamuenzi kama shujaa pekee aliyefanya kazi nzito ya kuiangusha CCM iliyowashinda watu wanaojiona kuwa wana afya bora kuliko wenzao.