Watanzania tumechagua hili?

Zipuwawa

JF-Expert Member
Nov 28, 2010
3,051
653
TUMEAMUA KUWA WAJINGA?

UJINGA UNA FAIDA, UJINGA RAHA, UJINGA NI MAISHA MAREFU, TAZAMA NDOA ZINADUMU KWA SABABU MMOJA KAKUBALI KUWA MJINGA, TANZANIA INA AMANI KWA SABABU YA UJINGA WA WATANZANIA, LAITI GADAFI ANGEKUBALI KUWA MJINGA ASINGEKUFA, URAFIKI UNAODUMU NI ULE AMBAO MMOJA KAKUBALI KUWA MJINGA.

HATA HAPA JF WAJINGA TUKIONGEZEKA NI WAZI HATUJAKUJA KUFANYA LA MAANA KWANI KILA KITU TUTAKIONA KIZURI .JE UJINGA HUU UNARAHA GANI KWA WATANZANIA? TUENDELEE KUUKUMBATIA?

Ni wazi kuwa Watanzania Uvumilivu umezidi, mwisho wake ni Ujinga .....Kila kona matatizo na Watanzania wanafurahia maisha haya kwanini hatujiulizi? Kila kona matatizo leo kukicha kuna hili kesho hili lakini tunaendelea kuwa wavumilivu ili kulinda Amani ya Tanzania. MVUMILIVU HULA MBOVU hili ndio linalotukumba leo hii.


Angalia watu wanavyopata shida hivi leo hii haki hakuna lakini Watanzania Tumekaa kimya lini tutaamka? Serikali tuliyoiweka madarakani kwa lengo la kutuungoza kwa kufuata matakwa yetu leo wameamua kutusaliti. Mishahara inachelewa kwa wafanyakazi, Huduma za Jamii duni kila kona lakini watanzania tunaendeleza kuwa wavumilivu ni mpaka lini? kwani haya hatuyaoni?

NAWASILISHA KWA WANAJF .........................!

  • :poa


 
Back
Top Bottom