share
JF-Expert Member
- Nov 22, 2008
- 6,062
- 10,461
Ukienda tutahesabiwa mauti, ukirudi tutahesabiwa ushindi.Mungu akitaka kuuangusha utawala wa kidhalimu, hua anatumia vizazi vyao wenyewe.
Kuna mifano mingi, ila mmoja kwa dini zote;
Mtume Mosses (Nabii Mussa A.S) alilelewa na farau wa misri, ndani ya familia na ndani ya kasri lake. Kipindi ambacho farau aliambiwa na waganga wake kwamba kuna mtoto wa kiume amezaliwa kuja kumaliza maisha yake na kuuangamiza utawala wake milele.
Baada ya kuambiwa tu, aliamua kuwachinja watoto wote waliozaliwa na wanaozaliwa wote wa kiume, na akawaacha watoto wa kike.
Ila Mtume Mosses (Nabii Mussa A.S) alizaliwa, na mungu kuonesha uwezo wake, alifanya alelewe ndani ya kasri la farau mpaka akakua. Alikwepeshwa na yale mauwaji ya watoto wa kiume maelfu kwa maelfu. Kisha ahadi ikatimia ya kumuangamiza farau kupitia kwake.
Tuje TANZAGIZA;
Tanzania, wameuliwa, wamefungwa, wameonewa na kupotea watu wengi sana kwa hofu ya kuja kuangamiza utawala wa kifarau (CCM), kina Ben Saanane, Azory Gwanda na kadhalika. Ila kuna mmoja tu ambae ameshindikana, Tundu Lissu. Sijui inaashiria nini hasa wana bodi.