Watanzania na Kutetea maovu

Watanzania na Kutetea maovu

Life2

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2016
Posts
3,377
Reaction score
4,847
Hii kasumba ipo sana miongoni mwa Watanzania, zamani ilikua ni kwenye vijiwe vya kahawa.

Hatimaye imekua Kansa sugu, taasisi za kidini, vyama vya siasa, vyombo vya ulinzi, viongozi wakubwa wa nchi wastaafu na wasasa, vijana, wazee, Radio na hata mitandao ya kijamii.

Kwa sasa ni kitu cha kawaida maovu kutetewa kwa nguvu kubwa mnoo, je tatizo ni umaskini wetu au?

Ukitaka kupendwa kwa sasa Tanzania wewe tenda maovu.

Iba kura

Piga watu wasio na hatia risasi

Teka na poteza watanzania

Wape ndugu zako vyeo kiharamu.

Finya haki za wafanyaki.

Kamata wapinzani weka ndani bila kesi

Sema uwongo uwongo...nk

Ukiwa shujaa wa hayo mambo zitajitokeza taasisi za dini zitakutetea, watakuja viongozi wa dini watasimama na wewe na wengine hata kutishia kuchinja wenzao, watasimama vyombo vya usalama watakutetea, kabla hakujapoa watakuja wana siasa, wanamichezo, machawa Pro max, vyama vya bodaboda, bajaji, Tax, na mbaya zaidi hata wanasheria na wao watakutetea.

Hivi ni kwamba watu wanakua hawafahamu ukweli au ni kujizima data tu haiwezekani dunia nzima wanasema flani muovu halafu wewe kutwa kucha kuwatetea.

Ni lini hii kasumba itakwisha na watanzania kuzungumza ukweli na kuacha kutetea maovu?

Kama wewe ni mmoja wao hebu badilika ili hata siku ukifa uwache historia nzuri duniani na si watu kuanza kushangilia kifo chako.
 
Shida ni njaa bro.
Kuna watu wapo tayari kutetea maovu ili mradi wanalipwa pesa.

Watenda maovu: majizi, mafisadi, watekaji, wafiraji, wauaji, nk hulipa pesa kwa majinga kuwatetea
 
NI hatari sana na mbaya zaidi unapatakana na wasomi kabisa wapo mstari wa mbele kutetea chinjachinja maovu
Shida ni njaa bro.
Kuna watu wapo tayari kutetea maovu ili mradi wanalipwa pesa.

Watenda maovu: majizi, mafisadi, watekaji, wafiraji, wauaji, nk hulipa pesa kwa majinga kuwatetea
 
There is every reason and every circumstance to declare that CCM is not a political party; CCM is a terrorist organization. From now on, the world must place it on the list of terrorist organizations.
Ccm is the ruling party of Tanzania government under Samia Suluhu hassan
 
Ukiwakosoa wanasema una chuki nao, unataka kuharibu amani ya nchi, hawataki kujua kuna haki, na wao ndo wameharibu kwa asilimia zote
 
Shida ni njaa bro.
Kuna watu wapo tayari kutetea maovu ili mradi wanalipwa pesa.

Watenda maovu: majizi, mafisadi, watekaji, wafiraji, wauaji, nk hulipa pesa kwa majinga kuwatetea
 
Back
Top Bottom