BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,283
Mandela ni sinema mpya iliyotoka hivi karibuni kuhusu maisha ya Mandela tangu alipoamua kujiingiza kwenye mambo ya siasa hadi anashinda katika uchaguzi wa Urais katika uchaguzi uliofanyika 1994 kama sikosei, title yake ni Long walk to freedom. Bila kupambana na mfumo dhalimu unaozidi kuota mizizi nchini udhalimu dhidi ya Watanzania walio wengi utazidi kuongezeka kwa kasi ya kutisha. Angalia operesheni Tokomeza jinsi watu walivyoteswa, kutiwa vilema na wengine kuuwawa na mali zao chungu nzima kuharibiwa. Haya yametokea pia kule Mtwara. Vyombo husika vya kuweza kupambana na hawa Wachina ili kuhakikisha sheria za nchi zinafuatwa vimeamua kuangalia pembeni na huku udhalimu ukizidi kupamba moto. Wanaweza kwenda pale wakakatiwa rushwa kidogo hao wanaondoka zao na udhalimu ukizidi kushamiri nchini. Watanzania kule China kamwe hawawezi kuwanyanyasa wachina kiasi hiki, kwanini sisi tukubali Watanzania wenzetu wanyanyaswe hadi wanaanza kufa kazini kutokana na unhealthy working conditions.
Ndugu yangu BAK haya mbona yanatendeka sana ukianzia huko kwa wahindi ndio usiombe bado migodini kuna mengi huko. Hebu njuze mandela nini hiyo mbona hapa umeniacha kwenye mataa.