Watanzania hatujui kiswahili wala kiingereza

Ozzie

JF-Expert Member
Oct 9, 2007
3,217
1,259
Nimekuwa napata shida sana kuzielewa taarifa au michango toka katika magazeti mbalimbali hapa Tanzania na hata pia humu ndani ya JF. Baadhi ya makala ili uzielewe inatakiwa ujitahidi mwenyewe kuumba maneno na sentensi kama wafumbua fumbo. Mara nyingi lugha ya kiswahili huwa haitumiki kwa usanifu na usadifu. Na hata wanaochagua kutumia kiingereza huwa hawajali kama wametumia maneno sahihi ukiachia mbali mambo ya 'structure'.
Utashangaa mtu anaandika 'ajui' akiwa na maana 'hajui', 'akuwepo' akiwa na maana hakuwepo n.k. Pia sheria ya kuanzia herufi kubwa baada ya nukta haitumiki hasahasa watu wanapochangia hoja fulani. Hii ni mifano midogo katika matumizi mabaya ya lugha. Nashangaa inakuwaje twashindwa kutumia lugha vizuri, japo wengi wa wanaotumia lugha vibaya wanaonekana ni wasomi wazuri maana hoja zao huwa zimeshiba.
Binafsi si mtaalamu wa lugha, ila ninajitahidi kujifunza. Naamini hata makosa yakiwa ni madogodogo, hakika yataondoa imani ya hoja au ujumbe unaotolewa kwa kuwa yatakuwa yametoka kwa mtu asiye makini.
 
Nimekuwa napata shida sana kuzielewa taarifa au michango toka katika magazeti mbalimbali hapa Tanzania na hata pia humu ndani ya JF. Baadhi ya makala ili uzielewe inatakiwa ujitahidi mwenyewe kuumba maneno na sentensi kama wafumbua fumbo. Mara nyingi lugha ya kiswahili huwa haitumiki kwa usanifu na usadifu. Na hata wanaochagua kutumia kiingereza huwa hawajali kama wametumia maneno sahihi ukiachia mbali mambo ya 'structure'.
Utashangaa mtu anaandika 'ajui' akiwa na maana 'hajui', 'akuwepo' akiwa na maana hakuwepo n.k. Pia sheria ya kuanzia herufi kubwa baada ya nukta haitumiki hasahasa watu wanapochangia hoja fulani. Hii ni mifano midogo katika matumizi mabaya ya lugha. Nashangaa inakuwaje twashindwa kutumia lugha vizuri, japo wengi wa wanaotumia lugha vibaya wanaonekana ni wasomi wazuri maana hoja zao huwa zimeshiba.
Binafsi si mtaalamu wa lugha, ila ninajitahidi kujifunza. Naamini hata makosa yakiwa ni madogodogo, hakika yataondoa imani ya hoja au ujumbe unaotolewa kwa kuwa yatakuwa yametoka kwa mtu asiye makini.

Ama hakika hapo umeongea ukweli mtupu. Mfano vituo vya redio ndio balaa..watangazaji wanaropoka tu .. yaani kwa kweli inakera sana! Kizazi cha sasa sijui tukiiteje maana kiswahili sifuri na kiingereza sifuri!
 
Ama hakika hapo umeongea ukweli mtupu. Mfano vituo vya redio ndio balaa..watangazaji wanaropoka tu .. yaani kwa kweli inakera sana! "(KIZAZI CHA SASA SIJUI TUKIITEJE)" maana kiswahili sifuri na kiingereza sifuri!

Daah! amakweli!! Unaoja mkubwa make watangazaji redio utumia maneno kimakosa kama vile mashule, masweta namjua badala ya fahamu mbayazaidi wanachanganya wasikilizaji kwa kutumia lugha 2,hiki kiite kizazi cha nyoka au ukipunguzamakari bas sema kizazi cha doti(.)com
 
Daah! amakweli!! Unaoja mkubwa make watangazaji redio utumia maneno kimakosa kama vile mashule, masweta namjua badala ya fahamu mbayazaidi wanachanganya wasikilizaji kwa kutumia lugha 2,hiki kiite kizazi cha nyoka au ukipunguzamakari bas sema kizazi cha doti(.)com

Mkuu, hata wewe unahitaji kuwa makini na kujifunza kiswahili kizuri zaidi.
 
Kweli kabisa.
Lugha zote mbili hatuzijui vizuri na watu wanavyochapia ndo kabisa.
Kuna mmoja humu aliandika 'hiv' kumbe amemaanisha HIV.
Kazi kwelikweli.
 
Kweli kabisa.
Lugha zote mbili hatuzijui vizuri na watu wanavyochapia ndo kabisa.
Kuna mmoja humu aliandika 'hiv' kumbe amemaanisha HIV.
Kazi kwelikweli.
Hiyo ipo hata kwangu kdg kdg!
Naona itakua twaiga mahala fulani.
Kama umemuelewa mwanzishi wa hii thread....ujitahidi mwenyewe kuweka mambo sawa!.
 
Back
Top Bottom