Watalaamu na Wabobezi wa meditation hii imekaaje?

Wang Shu

JF-Expert Member
Feb 1, 2014
2,563
3,708
Wakuu salaam

Nimekuwa mtu wa kujaribu kwa vitendo hili zoezi mara kwa mara katika siku tofauti nimelifanya takribani siku 8, sio siku zote mfululizo.

Muda ninaofanya meditation kuanzia saa 7 usiku hadi saa 10 kwa maeneo niliyopo huu muda ni rafiki na tulivu sana.

Nilifanya siku 4 mfululizo lakini nilishindwa kutuliza akili na mawazo sehemu moja, nikajipa likizo kama wiki moja nikiwaza nashindwaje nikapitia baadhi ya thread nikaongeza maarifa.

Kwa mara ya tano baada ya wiki kupita nilijiandaa tangia asubuhi nikajisemea kuwa leo usiku nitafanya meditation na ilipofika usiku eneo lilikuwa linanisubiri mimi tu nianze.

Siku hiyo ya tano ilikuwa ya tofauti sana tena sana nilifanikiwa kirahisi, ndio niliona matokea ya meditation lakini nilishindwa kuvumilia kutokana na vitu nilivyokuwa nahisi mwilini na kuona hali nisiyoilewa.

Mwili wangu uliganda nilikuwa kama nimechomwa sindano ya ganzi siwezi kuinua hata kidole macho pia nilishindwa kufumbua vitu vinaingiliana yaani sielewi mapigo ya moyo yakienda mbio sana, nilikuwa kama nazungushwa kwenye kiti.

Ilinikuta hofu kwa hali ile nikaanza kujaribu kutoka niache ilikuwa ngumu kiasi maana sikuweza kujifanyia chochote, lakini baadaye nilifanikiwa na sikuendelea lakini niliona mabadiliko makubwa sana, mwili mwepesi na baada ya hapo nililala usingizi mzito, nikasema mwanzo mzuri.

Kwa mara ya 6 siku iliyofuata nilifanya tena nikashindwa tena sikufikia hata robo ya siku iliyopita, niliendelea kurudia siku 3 mfululizo lakini nilishindwa kabisaa nimeshindwa kujua tatizo.

Mazingira ni yaleyale nafanya gizani nikiwa nimekaa mkao uleule wa siku niliyofanikisha lakini nashindwa kuupata mwendelezo wake.

Kwa sasa nimejipa muda wakupumzika sifanyi lakini naitaji kujua hii imeekaje nifanya nini? Niongeze kitu gani?
ili niendelee kuyaona matokeo kama yale au zaidi!!?

Nawasilisha..
 
Meditation ni kitu gani mkuu?
Mkuu kwa kiswahili ni "kutafakari"
Unatuliza mwili na akili,
Kwa maelekezo zaidi tafuta thread zake utaelewa
images-1.jpg
images.jpg
 
Yaani mimi sina stori kila nikipitia thread zake humu natamani nibobee lakini kila siku ni kama mwanafunzi, japo sikati tamaa lakini mafanikio ya haraka siyaoni ni mwezi wa3 natafuta mafanikio nipo hatua za mwanzo kabisa njia nimezielewa nafanya hii ya kuhesabu pumzi nikiona haiendi hii mara kuangalia kitu kimoja lakini bado sana
 
Mimi sio mtaalamu nimejifunzia humu humu na kinachokutokea kilinitokea nikwamba naona unataka ufike haraka kule ulipoishia lakini the key ni kupitia proces nzima whether ni ya pumzi au nyingine....focus focus .....mwenyewe ilinitokea kipindi nilivyovibrate at first nilipata shida iyo kwa wiki kadhaaa ila kwenye kusoma soma vitabu nikakutana na quote inayoelezea lazima uutafute utulivu kwanza usiwe na haraka...niko tayari kusahihishwa
 
Kwa navyo mimo japo ni beginner kama wewe na sina mentor na kwa. Uzoefu wangu binafsi.


Nakaa kwenye pozi la meditation naanza zoezi mawazo yanakuwa yanakuja mbalimbali mengi tu tofauti tofauti.

Mi nachofanya nayaangalia tu sifanyi kitu kadri mda unavyozidi kwenda yanaanza kupungua baada naanza kusikia hadi sauti ya ukimya kuna sauti inatokea kukiwa kimya kabisa hapo hata pumzi zako huzikii basi unaanza kupata ukimya km dk 3 wazo moja linakuja maraa ukimya mara wazo moja. Kuna kipindi mawazo hayaji kabisa nasikia nziiiiiiiiiiiiii

Ule ukimya kuna namna unakufanya uwe na amani sana.Sometimes uwaga kwenye paji la uso wangu inatokea duara kama la zambarau hivi....

Faida nilizopata kubwa mi ninavyoona ni uoga na hofu vinapungua,napunguza kula ovyo na kikubwa zaidi mawazo yangu ni kama yapo tofauti na mimi naweza kuyaona mawazo yangu kwa mbali.

Najaribu sana kupata mentor Iringa huku ila nakosa hivyo uwaga na enjoy utulivu wa nafsi na kucontrol mawazo yangu..

Interest yangu kubwa ni ku protect my energy na kudirect napopataka.
 
Kutoka kupiga ramli na kutii mizimu,
Umeanza kufata amri za tv na simu,
na ubaya ni kwamba umeikacha sanaa,
na kuanza kuifata siasa ambayo inakulaza na njaa,
kila unachokiona unataka kubeba, vichache vimekushinda na unataka kuongeza,
Juzuu, Kateksimu mpaka novena (not sure) vyote sio vyako,
Vyako vilikuwa kutamba ngonjera.

Nikwite nani mwafrika mzungu au mzungu mweusi?.Eti wewe mzee wa meditation, wewe ni mwafrika mchina au mchina mweusi?
 
Labda sasa kuna mahali sikuelewa binafsi mawazo/fikra zikija au zile picha huwa nazipuuza na kutaka kubaki empty sijajua kama ndio nipo sahihi au na lengo ni kubaki kuhesabu pumzi tu au nikae kimya bila kuwaza kitu
 
Kutoka kupiga ramli na kutii mizimu,
Umeanza kufata amri za tv na simu,
na ubaya ni kwamba umeikacha sanaa,
na kuanza kuifata siasa ambayo inakulaza na njaa,
kila unachokiona unataka kubeba, vichache vimekushinda na unataka kuongeza,
Juzuu,Kateksimu mpaka novena(not sure) vyote sio vyako,
Vyako vilikuwa kutamba ngonjera.

Nikwite nani mwafrika mzungu au mzungu mweusi?.Eti wewe mzee wa meditation, wewe ni mwafrika mchina au mchina mweusi?
😂😂😂😂 mimi ni mtanzania.
 
Labda sasa kuna mahali sikuelewa binafsi mawazo/fikra zikija au zile picha huwa nazipuuza na kutaka kubaki empty sjajua km ndo nipo sahihi au na lengo ni kubak kuhesabu pumnzi tu au nikae kimya bila kuwaza kitu
iyo ndio kazi kubwa kuifanya akili isiwaze kitu Kimoja au isiwaze kabisa
 
Kwa navyo mimo japo ni beginner kama wewe na sina mentor na kwa. Uzoefu wangu binafsi.


Nakaa kwenye pozi la meditation naanza zoezi mawazo yanakuwa yanakuja mbalimbali mengi tu tofauti tofauti.

Mi nachofanya nayaangalia tu sifanyi kitu kadri mda unavyozidi kwenda yanaanza kupungua baada naanza kusikia hadi sauti ya ukimya kuna sauti inatokea kukiwa kimya kabisa hapo hata pumzi zako huzikii basi unaanza kupata ukimya km dk 3 wazo moja linakuja maraa ukimya mara wazo moja. Kuna kipindi mawazo hayaji kabisa nasikia nziiiiiiiiiiiiii

Ule ukimya kuna namna unakufanya uwe na amani sana.Sometimes uwaga kwenye paji la uso wangu inatokea duara kama la zambarau hivi....

Faida nilizopata kubwa mi ninavyoona ni uoga na hofu vinapungua,napunguza kula ovyo na kikubwa zaidi mawazo yangu ni kama yapo tofauti na mimi naweza kuyaona mawazo yangu kwa mbali.

Najaribu sana kupata mentor Iringa huku ila nakosa hivyo uwaga na enjoy utulivu wa nafsi na kucontrol mawazo yangu..

Interest yangu kubwa ni ku protect my energy na kudirect napopataka.
Unafanikiwa kila inavyofanya?
 
Yaani mi sina stori kila nikipitia thread zake humu natamn nibobee lakini kila siku ni km mwanafunzi,japo sikati tamaa lkn mafanikio ya haraka siyaoni ni mwezi wa3 natafuta mafanikio nipo hatua za mwanzo kabisa njia nimezielewa nafanya hii ya kuhesabu pumnz nikiona haiendi hii mara kuangalia kitu kimoja lkn bado sana
Yaani mi sina stori kila nikipitia thread zake humu natamn nibobee lakini kila siku ni km mwanafunzi,japo sikati tamaa lkn mafanikio ya haraka siyaoni ni mwezi wa3 natafuta mafanikio nipo hatua za mwanzo kabisa njia nimezielewa nafanya hii ya kuhesabu pumnz nikiona haiendi hii mara kuangalia kitu kimoja lkn bado sana
ipo siku utapatia mkuu
 
Ngoja niwatishe!

Naona mnataka ID zenu tuziandikie RIP!... 😅

Mwana kulitafuta mwana kulipata..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom