Wataalamu njooni hapa

Wataalamu njooni hapa

Kuletewa uji sio jambo baya…Just imagine kama akiwa na nia mbaya na wewe huoni ni fursa ya kukumaliza?
Kama hauna mahusiano mazuri na huyo jirani sidhani kama ataamua tu kukuletea uji na wewe ukajifanya kimbelembele kuupokea...
 
Umekosea sana mkuu, mtu mwenye Nia mbaya haji kwa staili hiyo, wakiamua kukuroga, unarogwa bila ya wewe kujua kama unarogwa. Omba msamaha kwa MUNGU.
 
Umekosea sana mkuu, mtu mwenye Nia mbaya haji kwa staili hiyo, wakiamua kukuroga, unarogwa bila ya wewe kujua kama unarogwa. Omba msamaha kwa MUNGU.

Bila mimi kujua eti
 
Jifunze kusema NO

Halafu majirani kupeana misosi ni kawaida sana,, ndio ujamaa aliotuachina nyerere huo...

Anyways ukiona hutaki basi uwe unakataa na sio unapokea halafu unaenda kumwaga.. Jasho la Mtu hilo
 
Kuletewa uji sio jambo baya…Just imagine kama akiwa na nia mbaya na wewe huoni ni fursa ya kukumaliza?
Mkuu embu toa kwanza hiyo avatar ya huyo mzee alafu tuanze kujadili mada yako.

Maana yeye kwenye uongozi wake aliwajali na kuwaheshimu sana watu wa hali ya chini kama walemavu na wajasiriamali na luouga nao picha sehemu mbali mbali za nchi,sasa wewe kuishi vizuri tu na huyo maskini ambaye ni jirani yako unashindwa mpaka ushindwe kunywa uji wake.
 
Inekugharimu kiasi gani kuukataa huo uji? Ukute wenyewe wamejihini ili washee na wewe kidogo chao, lakini kwa imani yako ya kishirikina umeenda kuumwaga.

Kiuhalisia hao watu ni matajiri kuliko wewe, maana wamekupa kidogo chao bila kuangalia hali yako kuwa pengine unacho zaidi yao.

Umaskini sio uchawi ndugu. Badili fikra yako la sivyo ipo siku utakutana na waliokuzidi kipato ambao watakuona na wewe maskini wakufanyie kama unavyowafanyia wenzako.
 
Wanajamii nahitaji msaada wenu kidogo…Mimi hapa ninapokaa kwa mbele kuna kanyumba ka uswahili sasa muda wa kufturu umefika nikaletewa uji,kuletewa nikaona aibu ikabidi nyinwe tu maana ningeonekana vipi kwa watu au labda na ringa…ule uji nimekunywa kama robo hivi kikombe,mwingine nimeingia home nikamwaga,na nikaenda chooni kutapika nikahakikisha uji wote umeisha…Swali langu,je kama mtu alikuwa na nia mbaya na mimi kupitia hicho kiwango kidogo cha uji anaweza nidhulu au nilivyojitapisha bado naweza dhulika? Wakuu nipeni muongozo,nakumbuka kwetu niliambiwa usipewe vitu vya kula kula hasa kwa watu usiowaamini
Tatizo ni hiyo Avatar yako
 
Hah dah eti kajumba ka uswahili,suala la uchawi Lina angle nyingi sanaa,unaweza kurogwa kwa njia nyingi...au unaishi kwa kujishtukia Nini?...jifunze kusema hapana au nimeshiba.
 
Hah dah eti kajumba ka uswahili,suala la uchawi Lina angle nyingi sanaa,unaweza kurogwa kwa njia nyingi...au unaishi kwa kujishtukia Nini?...jifunze kusema hapana au nimeshiba.

Watu wana mambo mengi mkuu sio kuamini kila mtu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom