Wastaafu wa PSPF wapewe kipaumbele

Aurora

JF-Expert Member
May 25, 2014
7,308
5,272
Habari Zenu Wapendwa

Hii Kauli mbiu ya Hapa Kazi tu, embu ifanyike kwa hawa wastaafu wa PSPF ambao inaendea mwaka sasa wanateseka bila kulipwa mafao yao.

Inajulikana kabisa pesa zao zilienda wapi, na kama zitarudi au hazirudi, hivyo basi Serikali ingechukua hatua stahiki ya haraka kufuta machozi ya hawa wastaafu.

Kitendo cha kukaa kimya bila kulitafutia ufumbuzi kinasikitisha sana, wazee hawa wameitumikia nchi yao kwa Moyo, na sasa muda wa kwenda kupumzika umefika,wanajibiwa kuwa pesa za kuwapa hazipo, si sahihi kabisa.

Wengine wamestaafu lakini bado wana majukumu ya kutunza familia zao, kutolipwa pesa zao mnawafanya waishi maisha yenye stress sana, yatakayoweza kuwapa magonjwa na hata kufupisha maisha yao.

Muwe na Siku njema
 
hili shirika ni tabu tupu yaaaani daaah! pale mtwara kuna uozo tu na ni waongo kupita wafanyakazi wa taasisi zingine hv hawa wanateuliwa na nani hasa yaaani daaah!
 
Back
Top Bottom