Jolebatawi
JF-Expert Member
- Dec 10, 2011
- 549
- 230
Hata HALIMA MDEE wakati anagombea jimbo la KAWE mpinzani wake tokea CCM alikuwa anabeza kwenye kampeni kwa kusema mashabiki wake na wanaokusanyika kwenye mikutano yake ni wahuni na wavuta bangi,Lakini mwisho wa siku jimbo ndiyo likabebwa na MDEE.Kwa mfano huo sishangai kwa sasa maoni yaliyotolewa na wananchi tena wengi yakibezwa na kuitwa majina mengi mara MAONI YA WAPINZANI,au MAONI YA UKAWA,au MAONI YA WACHACHE n.k,hamuwezi kuona wala kusikia sababu mmeshapigwa upofu ila mtakapokuja kustuka na kujua kumbe ilikuwa ni sauti ya wananchi na si ya wapinzani itakuwa IT IS TOO LATE!