Wasomi 1,500 wa Vyuo Vikuu wajiunga CCM

Wasomi 1,500 wa Vyuo Vikuu wajiunga CCM

Omary Kipingu

Member
Joined
Feb 22, 2016
Posts
40
Reaction score
48
LEO TAR 01/02/ 2018

*Kaimu katibu wa Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu* Ndg Daniel Zenda Leo amekabidhi kadi za Wanachama Uvccm 1500 kwa *katibu Hamasa Seneti ya Mkoa wa Dsm* Ndg Juakali kuwanya , Baada ya Mwamko mkubwa wa wanafunzi wa Vyuo Vikuu kuunga mkono na kuvutiwa na Utendaji Uliotukuka wa *Rais John Pombe Magufuli* na Serikali yake ya Awamu ya Tano na kuamua kujiunga na chama anacho kiongoza *Chama Cha Mapinduzi* na Jumuiya zake.

Imetolewa na
Uvccm Seneti Mkoa Dsm.
IMG-20180201-WA0145.jpg
 
Hii inahusiana nini na maisha ya watu masikini? Watu masikini wanaendelea kupata tabu lakini ccm yenyewe haijali bali kununua wapinzani.
 
Ni wasomi au vichomi wa vyuo vikuu? Ukweli ni kwamba Vijana wa CCM Vyuo Vikuu huwa hawajui, ufaulu wao ni GPA za chini ya 2.5...ndo akina Makonda, na bado wanataka tuwatambue kuwa ni wasomi?
 
Je kwa sasa na vyama vngine vinaruhusiwa kufika vyuo vikuu vikatafute wanachama kama inavyoruhusiwa uvccm? Ukijibu hili swali ndo ntapongeza kwa kupata wanachama hao 1500.
 
UVCCM tumeshazoea kwa kupika takwimu. Hii mpaka aje Msando athibitishe isije ikawa muendelezo wa janja janja ya kumdanganya mwenyekiti.
 
Siwezi kushangaa maana wasomi wengi ndio waliotufikisha hapa tulipo.Viongozi wengi ni wasomi lakini angalia mikataba mibovu waliyoisain.Kama Udsm kwenye maprofesa nguli mwekezaji anakuja na USD 75 nini maana yake?Bado mikataba kibao mibovu ambayo imesainiwa ya hovyo hovyo na wasomi hao hao.Wasomi wengi wasiojitambua ni wachumia tumbo tu.Kwa mtu anayefikiri kwa umakini miaka zaid ya hamsini ya uhuru bado tunatapatapa kwenye maendeleo na rasilimali kibao tunazo zinabebwa tu na wajanja wachache huwez kuwapenda hawa jamaa wa Lumumba!
 
Kama wewe ni omary kipingu ninayekufahamu , hebu niulizie hao jamaa kwamba Kazi wamepata ?
 
Hebu nikae pembeni kidogo nisikiizie kutoka kwa upande mwingine
 
Msomi anayechukua upande kwenye siasa ni msomi wa kutiliwa shaka kwa sababu, kwa aina ya siasa zetu, atatakiwa ashangilie kila kitakachofanywa na chama chake hata kama ni cha kipumbavu na aponde kila kitakachotoka upande hasimu hata kama kina tija kwa taifa.

Na kama katika kuchukua upande huo unakuwa upande wa oppressors unageuka kuwa kituko zaidi kumlinganisha na yule anayechukua upande wa wanaokandamizwa. Hivi ni msomi wa aina gani anayeweza kushangilia kuona ukandamizwaji wa upinzani huku kukiwa na dalili ya kuleta political monopoly?

Hivi ni msomi wa aina gani asiyeweza kuogooa kuona nia ya CCM kutaka ibaki peke yake kwenye siasa za Tanzania?!

Nilitarajia vijana wadogo kama hawa wawe ndio chachu ya kupigania taifa kuliko kuwa sehemu ya kupigania chama.
 
Na watawapatia kazi kabisa. Kama waliowatangulia kuwa CCM vyuoni.
 
Back
Top Bottom