Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira amesema chama hicho hakikuundwa ili kuwa chama cha muda bali kiliundwa ili kuwa chama cha kudumu
Akizungumza leo Mei, 28 2025 wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa jengo jipya la Makao Makuu ya CCM mkoani Dodoma Wasira amesema “chama chetu kilipoanzisha tuliweka kaulimbiu tunasema kidumu Chama cha Mapinduzi maana yake hakikuundwa kuwa chama cha muda kiliundwa kuwa chama ha kudumu”
"Na viashiria vya kudumu kwa Chama cha Mapinduzi ni kuwa na vijana na kwa hiyo kitakuwa kinadumu kupitia vijana" ameongeza Wasira
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Aidha ameeleza kuwa uamuzi wa kuweka jiwe hilo la msingi ni utekelezaji wa maono ya kuwa na mahali ambapo chama hicho kitakuwa na anuani ya kudumu.
Akizungumza leo Mei, 28 2025 wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa jengo jipya la Makao Makuu ya CCM mkoani Dodoma Wasira amesema “chama chetu kilipoanzisha tuliweka kaulimbiu tunasema kidumu Chama cha Mapinduzi maana yake hakikuundwa kuwa chama cha muda kiliundwa kuwa chama ha kudumu”
"Na viashiria vya kudumu kwa Chama cha Mapinduzi ni kuwa na vijana na kwa hiyo kitakuwa kinadumu kupitia vijana" ameongeza Wasira
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Aidha ameeleza kuwa uamuzi wa kuweka jiwe hilo la msingi ni utekelezaji wa maono ya kuwa na mahali ambapo chama hicho kitakuwa na anuani ya kudumu.