Wasipokuwa makini kwa hili nchi itajigawa kimakundi

Hata sielewi, hivi lile basi la washabiki wa Yanga linalochanja mbuga huko zambia kuelekea kwa Mandela limegharamikiwa na serikali?
Yes kwa kila kitu, msimu uliopita Yanga walipewa ndege kwenda Algeria wakati huo Simba walijilipia kwenda Morocco,
Yanga walipelekwa Malawi.
Msimu uliopita kwenye michuano ya kimataifa mashabiki wa Yanga walikuwa wakinunuliwa tickets za mafungu na viongozi wa serikali ilihali Simba waliendelea na utaratibu wao wa kawaida.

Hawajui kuwa Simba ni half ya nchi na ndiyo inayobeba watu wengi ambao ni antagonistic wa mfumo tangu friends of Simba ?
 
Kwa akili zako unadhani nchi nzima zaidi ya watu 60+ni eidha simba au yanga sio??

Wengi hawana hata hiyo habari ya Yanga kulipiwa, na mashabiki wengi wa bongo hawafatilii hizo mbaga za ndani ni zile za juu juu tu.

Wewe kajua yote ndo unaumia kwasababu ya ufokonyoko wa kutaka kujua mengi.
 
Mnataka hela za serikali kwa nini? Embu achaneni na mambo ya serikali na mambo ya kisiasa haya
 
Habari Jr

Hoja ni fupi mno simba sc wanasafiri kesho alafujiri na inaondoka na mashabiki 17, hawa mashabiki wanaenda kujilipia wenyewe kila kitu.

Serikali muwe seriously na hii kitu mnaingiza siasa kwenye mpira,mashabiki wengi wa mpira hususani mashabiki wa Simba wameumia kitendo cha kumpendelea mmoja.

Mwisho msipokuwa makini mpira kuupeleka kwenye siasa mnaenda kugawa mashabiki kupitia Serikali.

Fikra zangu huwa zinaona mbali kama nilivyoona mh Paul makonda kuwa raisi 2030.
Haya mwisho imeharibu hata kile kidogo ulichokuwa unacho.
 
Hata mimi nimeona hili
Huwa nakiona Una akili kumbe huku kwenye Mpira wote mnageuka hamnazo.

Dar to Johannesburg ni kilometers 5000 tu, NI kama kutoka Dar kwenda Kigoma na kurudi na Kilometres kadhaa tu.

Mkiongea vizuri na wenye mabasi watawapeleka Kwa reasonable price.

Sasa serikali itowe ndege kadhaa kuwafurahisha Simba kwenda Cairo? Unajuwa gharama yake?

Huu ni wivu wa kipuuzi Kijiografia tupo karibu na South Africa na tuna maingiliano.

Haya Wana Simba tuonesheni basi lipi linalokwenda Cairo tuwalipie nauli?
 
Ndio shida serikali kujiinga kwenye vitu vya kipuuzi,mnalipia mashabiki wakati kuna wanafunzi wanakaa chini,
Serikali inaingia gharama kulipa wenza wa wastaafu, watu kujiongezea maposho hovyo.
Hii nchi ni kama ina laana vile.
 
Yes kwa kila kitu, msimu uliopita Yanga walipewa ndege kwenda Algeria wakati huo Simba walijilipia kwenda Morocco,
Yanga walipelekwa Malawi.
Msimu uliopita kwenye michuano ya kimataifa mashabiki wa Yanga walikuwa wakinunuliwa tickets za mafungu na viongozi wa serikali ilihali Simba waliendelea na utaratibu wao wa kawaida.

Hawajui kuwa Simba ni half ya nchi na ndiyo inayobeba watu wengi ambao ni antagonistic wa mfumo tangu friends of Simba ?
Yanga walienda Algeria kucheza mechi gani na Simba walienda Morocco kucheza mechi gani? usiwe unaongea bila kukamilisha sentence
 
Na kwa kupendelea Simba na Yanga mimi Mshabiki wa Lipuli niseme nini ? Ingawa ni kweli hii serikali imeshindwa kufanya kazi zake za maana (Umeme, Ugumu wa Maisha, Ajira zenye Ujira) wanaingilia mambo ambayo yapo sawa wala hayahitaji msaada wao (ili kujizolea Ujiko)
 
Inafikirisha kuona watu wanaojisifia eti wao ni wenye nchi na siyo wananchi kama Yanga wakianza kulia lia, kisa tu mashabiki wa timu ya upande wa pili wamegharamiwa na serikali baada ya kujiongeza na kuomba msaada!

Na nyinyi si mngeomba kama walivyofanya wenzenu! Au mlitaka kusaidiwa pasipo kuomba? Acheni kulilia vitu vidogo aisee! Mjue nyinyi ni watu wazima!!
Ukweli mtupu, ingekuwa ni wao wala kusengekuwa na maneno mengi.
 
Fikra zangu huwa zinaona mbali kama nilivyoona mh Paul makonda kuwa raisi 2030
Nimeshangaa fikra zako hazijakuonyesha unaandika utumbo mbele ya Great Thinkers. Serikali haijaweka upendeleo wowote ni viongozi wenu hawakua makini baada ya serikali kusema inasubiri timu ziseme zinataka serikali iwasaidie wapi!! Mtaisingizia serikali inapendelea ila kiukweli ni umakini na ufasaha wa viongozi wa Yanga ndio mnaona serikali inafanya upendeleo
 
Sasa kama hamjaandika barua ya kuomba msaada Msigwa atafanyia kazi barua gani
Kuweni serious basi
 
Mechi za nyumbani wanaingizwa bure,ugenini wanalipiwa,hii timu ina mashabiki mashoga
 
Back
Top Bottom