Wasiojulikana wanajulikana

Wasiojulikana wanajulikana

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,648
Reaction score
10,843
Unaposema wasiojulikana, ni muhimu kuweka maelezo sawa kuwa wasiojulikana kwa nani!

Hawawezi kuwa wasiojulikana kwa waliowatuma!

Hawawezi kuwa wasiojulikana kwa vyombo vya dola! Vinginevyo, tungeamini kuwa tuna vyombo vya dola vya hovyo kupitia kiasi. Vyombo vya dola vinawajua lakini havina la kuwafanya zaidi ya kuwasaidia pale wanapohitaji support yao!

Iweje waitwe wasiojulikana ilhali wanatumia mpaka miundo mbinu ya umma kutelekeleza uharamia wao?

Iweje waitwe wasiojulikana wakati ni wazi kabisa kuwa Polisi wanajitahidi kujiepusha nao?

Wasiojulikana kivipi wakati si majambazi? Wakiteka hawahangaika na mali za mtekwaji, bali maisha yake na hali yake tu! Wasiojulikana wanapata wapi hela ikiwa hawahangaika na mali za mtu wanayemteka?

Hawawezi kuwa vibaka, vinginevyo wasingehangaika na watu wa aina fulani pekee!

Siyo kweli kuwa ni wasiojulikana! Wanajulikana kwa kuwa ni "maprofessional" katili walioandaliwa na "watu" fulani kwa malengo yao haramu! Watu pekee wasisowajua ni ambao waliowaandaa "wasiojulikana" walipanga wasijue, ingawa wengi wameshajua!

Vipi wale waliomteka Sativa, walishajibu tuhuma zilizoelekezwa kwao? Au ndiyo vyeo vimeendelea kupanda?
 
Unaposema wasiojulikana, ni muhimu kuweka maelezo sawa kuwa wasiojulikana kwa nani!

Hawawezi kuwa wasiojulikana kwa waliowatuma!

Hawawezi kuwa wasiojulikana kwa vyombo vya dola! Vinginevyo, tungeamini kuwa tuna vyombo vya dola vya hovyo kupitia kiasi. Vyombo vya dola vinawajua lakini havina la kuwafanya zaidi ya kuwasaidia pale wanapohitaji support yao!

Iweje waitwe wasiojulikana ilhali wanatumia mpaka miundo mbinu ya umma kutelekeleza uharamia wao?

Iweje waitwe wasiojulikana wakati ni wazi kabisa kuwa Polisi wanajitahidi kujiepusha nao?

Wasiojulikana kivipi wakati si majambazi? Wakiteka hawahangaika na mali za mtekwaji, bali maisha yake na hali yake tu! Wasiojulikana wanapata wapi hela ikiwa hawahangaika na mali za mtu wanayemteka?

Hawawezi kuwa vibaka, vinginevyo wasingehangaika na watu wa aina fulani pekee!

Siyo kweli kuwa ni wasiojulikana! Wanajulikana kwa kuwa ni "maprofessional" katili walioandaliwa na "watu" fulani kwa malengo yao haramu! Watu pekee wasisowajua ni ambao waliowaandaa "wasiojulikana" walipanga wasijue, ingawa wengi wameshajua!

Vipi wale waliomteka Sativa, walishajibu tuhuma zilizoelekezwa kwao? Au ndiyo vyeo vimeendelea kupanda?
Na hapo sativa baada ya kusema wazi kuwa alitekwa badala ya kupatiwa msaada ndio kwanza polisi wanataka kumchukulia sheria kwamba analeta uchochezi
 
Watekaji hao nadhani wana mafunzo ya Ugaidi Si Ya Kipolisi au kijeshi kama ya vyombo vyetu vya dola.

Ihitimishwe kuwa Kuna Ugaidi Tanzania.
 
Watekaji hao nadhani wana mafunzo ya Ugaidi Si Ya Kipolisi au kijeshi kama ya vyombo vyetu vya dola.

Ihitimishwe kuwa Kuna Ugaidi Tanzania.
Hili mbona lipo wazi kabisa, ubabe umekithiri na hamna hatua zinazochukuliwa maana wahusika n hao hao wenye madaraka
 
Na hapo sativa baada ya kusema wazi kuwa alitekwa badala ya kupatiwa msaada ndio kwanza polisi wanataka kumchukulia sheria kwamba analeta uchochezi
Sheria ipi? Labda SHERIA MKONONI!

Wasingeweza kumshitaki!
 
Back
Top Bottom