Mubezi
Member
- Sep 27, 2010
- 71
- 23
Niliwaoji watu wa makamo kama 50 hv kila nilipohuzuria mikutano ya CCM hasa ya urais,kila mtu alikuwa na maoni yake ila yote yalilenga hapa,Ebu soma,"Ndugu zangu watanzania ni wazi kwamba kwa uchaguzi huu ndipo tunaweza kuchambua pumba tukazitupa na mchele wetu tukauweka ndani ya gunia ili kuwa chakula chetu kitamu cha baadae. Mgombea wa CCM na wapambe wake bado hawezi kutofautisha kati ya sera na ahadi kwa wapiga kura, Tangu siku ya kwanza ya kampeni hajamsikia akiongelea sera yoyote ya chama ndiyo maana imekuwa vigumu sana hata wagombea wa chama hicho kueleza sera kwa wananchi.Tunachokisikia ni ahadi na misaada na mikopo toka hapa na pale na mapicha mengi yaliyojaa gilba.
Sera ni kama kanuni ya chama kufutana na katiba ya chama husika ilivyo. na sera inapaswa imguse kila mwananchi kwa nchi nzima, tofauti ya ahadi ambazo zitawahusu watu wa Mafia tuu, sisi wa Iringa haituhusu. watu wa Kigoma tuu sisi wa Maswa haituhusu,mfano kuwapa wakulima pemebejeo,je wasio wakulima?. lakini Mgombea wa CHADEMA anapozungumzia elimu bure,cement kushuka bei, hiyo ni sera na itamhusu kila mwanachi, na Afya bure ni kwa kila mtu n.k., n.k.
Inaelekea CCM hawana sera ila uzushi na kukomalia mambo binafsi ya kuchafua wagombea wanaoonekana tishio kwa ufisadi. kuzusha Umwagaji damu na kufanya ndiyo sera yao labda iliwasaidia huko nyuma lakini kwa sasa sijui? mawefikia mwisho kwa hiyo mengi mtayaona na kuyasikia lakini watambue TZ ya leo si ya Jana watu wanataka mabadiliko".Hicho ndicho nilichokisikia kwenye mikutano ya ccm,ambacho wao CCm hawataki kukisikia.
Sera ni kama kanuni ya chama kufutana na katiba ya chama husika ilivyo. na sera inapaswa imguse kila mwananchi kwa nchi nzima, tofauti ya ahadi ambazo zitawahusu watu wa Mafia tuu, sisi wa Iringa haituhusu. watu wa Kigoma tuu sisi wa Maswa haituhusu,mfano kuwapa wakulima pemebejeo,je wasio wakulima?. lakini Mgombea wa CHADEMA anapozungumzia elimu bure,cement kushuka bei, hiyo ni sera na itamhusu kila mwanachi, na Afya bure ni kwa kila mtu n.k., n.k.
Inaelekea CCM hawana sera ila uzushi na kukomalia mambo binafsi ya kuchafua wagombea wanaoonekana tishio kwa ufisadi. kuzusha Umwagaji damu na kufanya ndiyo sera yao labda iliwasaidia huko nyuma lakini kwa sasa sijui? mawefikia mwisho kwa hiyo mengi mtayaona na kuyasikia lakini watambue TZ ya leo si ya Jana watu wanataka mabadiliko".Hicho ndicho nilichokisikia kwenye mikutano ya ccm,ambacho wao CCm hawataki kukisikia.