Shida za watu ni nyingi sana,haziwezi kutatuliwa kwenye mikutano ya viongozi

Twayemba

Member
Jan 29, 2024
12
14
Wapo viongozi wa kisiasa nchini mwetu,ambao wanaonekana kuguswa sana na matatizo ya mtu mmoja mmoja na hivyo kupenda kuwasikiliza hadharani kwenye mikutano yao ya kisiasa.

Hutokea watu wachache wakapata nafasi ya kujielezea shida zao,na kiongozi hutoa maelekezo na hivyo kuonekana shujaa kwa haraka.

Lakini kiongozi kushughulika na mtu mmoja mmoja,ni ngumu sana kwa sababu kila mwananchi anazo shida na kero zake ngumu kabisa. Hivyo kiongozi makini ni vizuri kushughulika na mifumo inayogusa watu wengi kwa wakati mmoja.

Aidha sifa kwa kiongozi mmoja mmoja sio tija kwa mwananchi,bali tija ni uwajibikaji wa serikali yote,au kama ni chama cha siasa inapendeza kuona jambo la chama linakuwa la viongozi wote na sio kiongozi mmoja.Enzi za kuhangaika na sifa kwa mtu mmoja, zilishapitwa.

Vyama vya siasa, viendelee kuelezea sera zao na serikali iliyopo madarakani iendelee kutekeleza wajibu wake kwa mujibu wa kanuni zilizopo.Kama kuna kunyosheana vidole, hayo wayafanye kwenye kikao vyao vya ndani.

Mbwembwe za kwenye majukwaa,ni vizuri zikabaki kwa wasanii wa muziki.
 
Kinacho tengenezwa ni bomu
Wakati wa kampeni za uchagizi Mkuu mtawadanganya Nini
Mmewafundisha kubeba mabango yamalalamiko
MudanimwLimu
 
Wapo viongozi wa kisiasa nchini mwetu,ambao wanaonekana kuguswa sana na matatizo ya mtu mmoja mmoja na hivyo kupenda kuwasikiliza hadharani kwenye mikutano yao ya kisiasa.

Hutokea watu wachache wakapata nafasi ya kujielezea shida zao,na kiongozi hutoa maelekezo na hivyo kuonekana shujaa kwa haraka.

Lakini kiongozi kushughulika na mtu mmoja mmoja,ni ngumu sana kwa sababu kila mwananchi anazo shida na kero zake ngumu kabisa. Hivyo kiongozi makini ni vizuri kushughulika na mifumo inayogusa watu wengi kwa wakati mmoja.

Aidha sifa kwa kiongozi mmoja mmoja sio tija kwa mwananchi,bali tija ni uwajibikaji wa serikali yote,au kama ni chama cha siasa inapendeza kuona jambo la chama linakuwa la viongozi wote na sio kiongozi mmoja.Enzi za kuhangaika na sifa kwa mtu mmoja, zilishapitwa.

Vyama vya siasa, viendelee kuelezea sera zao na serikali iliyopo madarakani iendelee kutekeleza wajibu wake kwa mujibu wa kanuni zilizopo.Kama kuna kunyosheana vidole, hayo wayafanye kwenye kikao vyao vya ndani.

Mbwembwe za kwenye majukwaa,ni vizuri zikabaki kwa wasanii wa muziki.
Sasa zitatatuliwaje?
 
Kama chama kime kaa madarakani miaka 63 na bado hakijui kina fanya nini Madarakani na bado mna kipa kura, nani mjinga?
Hivi Ccm ni ya kuzunguka mitaani kuulizia kero? Kweli??? Na watu mna jitokeza kutoa kero? Miaka 63 hawajui cha kuwa fanyia watanzania? Huu ni usanii wa kiwango cha lami.
 
Back
Top Bottom