Mzito Kabwela
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 18,857
- 7,617
LEO tumechapisha taarifa za wanafunzi wa kike wa Chuo cha Uandishi wa Habari Dar es Salaam (DSJ) kilichoko Ilala, Dar es Salaam, kuvamiwa na vibaka, wakaporwa mali, fedha na kisha kubakwa kwa zamu. Vibaka hawa wamepita kwenye lango linalodaiwa kuwa halifungwi muda wote.
Inadaiwa kuwa mlinzi aliyekuwa mlangoni, Mmasai alikamatwa akawekwa chini, akafungwa kamba, kisha vibaka hao wakaingia kwenye vyumba vya wanafunzi wa kike na kuanza kufanya maasi hayo. Hapa tunadhani yapo matatizo mengi kimsingi. Ukiacha uzembe kwa upande wa uongozi wa shule kutokuwa na lango imara, tatizo ni zaidi ya hilo.
Kwamba maelezo yaliyopo ndani ya habari hii, yanaonyesha muda tangu vibaka hao wamefika getini, wakapambana na Mmasai, kufunga kamba, kuingia tena katika vyumba vya hosteli kimoja baada ya kingine wakikusanya fedha, mali na kubaka mabinti hao, ulikuwa mrefu.
Katika eneo la ulinzi shirikishi, chuo kama hiki ambacho ni cha waandishi wa habari, tulitarajia hawa wangekuwa wa kwanza kuwasiliana na polisi. Hawa wangeweza kupiga simu polisi, wakaeleza hatari inayowakabili, na hakika polisi kwa sasa wana ushirikiano mkubwa, hivyo wangeweza kusaidia.
Lakini tunachokiona pia, Polisi sasa wanapaswa kuongeza kasi. Kinachotokea, ni kwamba wezi wa kutumia silaha nzito wamepungua, lakini idadi ya vibaka wenye kufanya wizi inazidi kuongezeka siku hadi simu. Jana usiku kucha, wananchi wa Kitunda, Ilala Dar es Salaam, walikesha wakifukuzana na vibaka.
Tena vibaka hawa wana jeuri kweli. Wanapita nyumba kwa nyumba wakigonga mlango na kuwataka wenye nyumba wafungue na kuwapa watakacho utadhani wanalipisha kodi. Kimsingi eneo kama Kitunda, wanapata athari za waliokuwa wakazi wa Kipawa, ambao wengi wamevunjiwa nyumba zao kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege, ambao wamemwagika Kitunda.
Tunasema vitendo vya vibaka kutumia nguvu kupora wananchi, tulikuwa tumevisahau. Kwa sasa hali hii imerejea kwa kasi ya ajabu, hivyo tunaliomba Jeshi la Polisi kurejesha utaratibu wa doria katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam. Tunaamini polisi wakifanya juhudi za makusudi, ni rahisi kukamata watu hawa wanaosumbua.
Kwa sasa vibaka wanavamia maduka ya kuuza vocha za simu, vibanda vya maji, lakini hatukutarajia waende hadi kwenye hosteli za wasichana na kufanya uasi wa aina hiyo. Tunataka hatua kali
zichukuliwe kuepusha aibu hii.
Source:
Polisi Dar changamkeni
Inadaiwa kuwa mlinzi aliyekuwa mlangoni, Mmasai alikamatwa akawekwa chini, akafungwa kamba, kisha vibaka hao wakaingia kwenye vyumba vya wanafunzi wa kike na kuanza kufanya maasi hayo. Hapa tunadhani yapo matatizo mengi kimsingi. Ukiacha uzembe kwa upande wa uongozi wa shule kutokuwa na lango imara, tatizo ni zaidi ya hilo.
Kwamba maelezo yaliyopo ndani ya habari hii, yanaonyesha muda tangu vibaka hao wamefika getini, wakapambana na Mmasai, kufunga kamba, kuingia tena katika vyumba vya hosteli kimoja baada ya kingine wakikusanya fedha, mali na kubaka mabinti hao, ulikuwa mrefu.
Katika eneo la ulinzi shirikishi, chuo kama hiki ambacho ni cha waandishi wa habari, tulitarajia hawa wangekuwa wa kwanza kuwasiliana na polisi. Hawa wangeweza kupiga simu polisi, wakaeleza hatari inayowakabili, na hakika polisi kwa sasa wana ushirikiano mkubwa, hivyo wangeweza kusaidia.
Lakini tunachokiona pia, Polisi sasa wanapaswa kuongeza kasi. Kinachotokea, ni kwamba wezi wa kutumia silaha nzito wamepungua, lakini idadi ya vibaka wenye kufanya wizi inazidi kuongezeka siku hadi simu. Jana usiku kucha, wananchi wa Kitunda, Ilala Dar es Salaam, walikesha wakifukuzana na vibaka.
Tena vibaka hawa wana jeuri kweli. Wanapita nyumba kwa nyumba wakigonga mlango na kuwataka wenye nyumba wafungue na kuwapa watakacho utadhani wanalipisha kodi. Kimsingi eneo kama Kitunda, wanapata athari za waliokuwa wakazi wa Kipawa, ambao wengi wamevunjiwa nyumba zao kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege, ambao wamemwagika Kitunda.
Tunasema vitendo vya vibaka kutumia nguvu kupora wananchi, tulikuwa tumevisahau. Kwa sasa hali hii imerejea kwa kasi ya ajabu, hivyo tunaliomba Jeshi la Polisi kurejesha utaratibu wa doria katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam. Tunaamini polisi wakifanya juhudi za makusudi, ni rahisi kukamata watu hawa wanaosumbua.
Kwa sasa vibaka wanavamia maduka ya kuuza vocha za simu, vibanda vya maji, lakini hatukutarajia waende hadi kwenye hosteli za wasichana na kufanya uasi wa aina hiyo. Tunataka hatua kali
zichukuliwe kuepusha aibu hii.
Source:
Polisi Dar changamkeni