kibaravumba
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 6,635
- 7,005
Awali tulibiambiwa maelekezo yote tutayapata kutoka kwa ama waziri wa Afya, Waziri Mkuu au Rais mwenyewe.
Pia, tuliambiwa tusikilize maelekezo ya wataalamu wa wizara ya Afya. Kauli hizi zilitolewa na viongozi wetu wakuu akiwemo mheshimiwa Rais.
Sasa naomba kuuliza swali hili,ni nani kwa sasa tumsikilize?
Baadhi ya wakuu wa mikoa wametangaza hatua za ziada zinazotakiwa kuchukuliwa.Mfano kuvaa barakoa kila unapotoka.
Awali msemaji wa wizara ya afya alisisitiza uvaaji wa barakoa sio muhimu kwa watu ambao hawajaambukizwa. Nakumbuka watu walishaanza kuvaa hizi barakoa bila hata amri kama zinazotolewa sasa. Na baada ya maelezo hayo tena ni daktari, waliovaa mitaani wakaonekana washamba tu. Leo wakuu wa mikoa (sio wasemaji wa huu ugonjwa) wanatoa maelekezo hayo.Tumsikilize nani?
Bado zinavaliwa masaa 4 zinatupwa? Na zikitupwa zinatupwaje? Au kuna sehemu zimeandaliwa za kutupa barakoa?
Vipi zilizotupwa zikizagaa mitaani, haziwezi kuwa chanzo cha kuenea kwa ugonjwa huu tena? Mamlaka zinajua uzito wa Ku-dispose barakoa zinazovaliwa kila baada ya masaa manne? Au watu wavae bila kujali masaa? Wasipozingatia masaa, nini kitatokea?
Kumbuka pia ukitoka masaa 8 kwa Siku ni barakoa 2 hizo ambazo ni sh. 2000@. Kwahiyo bajeti ya barakoa pekee ni sh. 4000@ siku. Kama ni mtumishi wa umma na unalipwa mshahara wa Shilingi laki nne, ujue kuna zaidi ya laki moja ya kununua barakoa pekee.
Tunaomba mwongozo tafadhali kutoka kwa wasemaji walioidhinishwa. Au hata kama kuna mabadiliko yamefanyika kuhusu wasemaji wa Covid-19
Sent using Jamii Forums mobile app
Pia, tuliambiwa tusikilize maelekezo ya wataalamu wa wizara ya Afya. Kauli hizi zilitolewa na viongozi wetu wakuu akiwemo mheshimiwa Rais.
Sasa naomba kuuliza swali hili,ni nani kwa sasa tumsikilize?
Baadhi ya wakuu wa mikoa wametangaza hatua za ziada zinazotakiwa kuchukuliwa.Mfano kuvaa barakoa kila unapotoka.
Awali msemaji wa wizara ya afya alisisitiza uvaaji wa barakoa sio muhimu kwa watu ambao hawajaambukizwa. Nakumbuka watu walishaanza kuvaa hizi barakoa bila hata amri kama zinazotolewa sasa. Na baada ya maelezo hayo tena ni daktari, waliovaa mitaani wakaonekana washamba tu. Leo wakuu wa mikoa (sio wasemaji wa huu ugonjwa) wanatoa maelekezo hayo.Tumsikilize nani?
Bado zinavaliwa masaa 4 zinatupwa? Na zikitupwa zinatupwaje? Au kuna sehemu zimeandaliwa za kutupa barakoa?
Vipi zilizotupwa zikizagaa mitaani, haziwezi kuwa chanzo cha kuenea kwa ugonjwa huu tena? Mamlaka zinajua uzito wa Ku-dispose barakoa zinazovaliwa kila baada ya masaa manne? Au watu wavae bila kujali masaa? Wasipozingatia masaa, nini kitatokea?
Kumbuka pia ukitoka masaa 8 kwa Siku ni barakoa 2 hizo ambazo ni sh. 2000@. Kwahiyo bajeti ya barakoa pekee ni sh. 4000@ siku. Kama ni mtumishi wa umma na unalipwa mshahara wa Shilingi laki nne, ujue kuna zaidi ya laki moja ya kununua barakoa pekee.
Tunaomba mwongozo tafadhali kutoka kwa wasemaji walioidhinishwa. Au hata kama kuna mabadiliko yamefanyika kuhusu wasemaji wa Covid-19
Sent using Jamii Forums mobile app