Kumekuwa na wimbi kubwa la wasanii wa Bongo fleva na Bongo Movie kushabikia CCM,tumeona wengi tena wale maarufu wakijitokeza waziwazi kwenye shughuli za CCM.Jambo la kujiuliza hivi ni kweli hawa wasanii wana mapenzi ya dhati na chama hiki au ni ubinafsi wao,au kwa kuwa wengi wao wana elimu ndogo hivyo kushindwa kuelewa matatizo makubwa yaliyosababishwa na CCM?