Wasanii huwa ni wahanga wa tawala nyingi duniani either negatively or positively

Wasanii huwa ni wahanga wa tawala nyingi duniani either negatively or positively

Matongee

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2023
Posts
1,226
Reaction score
3,173
Wakuu kabla ya kuwahukumu hawa viumbe tujikumbushe kuwa wasanii ni watu wenye ushawishi mkubwa kwenye jamii kuliko hata wanasiasa walio wengi. Kwa mfano Diamond peke yake ana ushawishi mkubwa kuliko wanasiasa wote wa nchi hii... kidunia hakuna Rais, mfalme au mtawala yeyote aliyekuwa akimzidi ushawishi hayati Michael Jackson kipindi akiwa hai.

Tawala karibu zote zinajua hilo ndo maana huwa zinawaweka karibu wasanii kwa kuwashawishi au kuwalazimisha kwa sababu kwa ushawishi walio nao ni hatari kuwaacha tu. Wakihamia kambi pinzani ni hatari kubwa. Wasanii wengi wamewahi kujikuta matatizoni kwa kusimama na itikadi tofauti na serikali iliyoko madarakani.

Mfano mrahisi ni majirani DRC zamani wakiitwa Zaire chini ya Dikteta Mobutu. Wasanii walipitia magumu kila walipokuwa wakionyesha misimamo yao inayokinzana na serikali. Hayati Franco aliwahi kukimbia nchi. Koffi Olomide mwaka 97 kama sio 98 aliwahi simamishwa barabarani na kushushwa kisha kucharazwa viboko na askari kama mtoto mdogo. Werrason alishushwa jukwaani akiwa anatumbuiza na kushushiwa kipigo cha mbwa mwizi. Kimsingi ni hatari kwa msanii kuwa na itikadi tofauti na serikali iliyopo madarakani. Hapa Tanzania mifano ipo na mnaijua.

Ninawasihi watanzania wote tusamehe hawa vijana kwa sababu wasingeweza kuepuka kukinywea kikombe walichokinywea.
 
Mkuu, waache hao wapuuzi

Wangekua wanafanya show, wanapiga pesa hafu wanakaa kimya tungejua ni wachakarikaji.

Tatizo linaanza wanaanza maneno ya kejeri na dharau mitandaoni.

Yaani wamevuka mipaka. Kusema kweli kwa upande wangu kuwasamehe ngumu sana

IMG_3031.png

Nimefuta nyimbo zao za recently zote nimebakisha old bongo fleva ambao 99% hawaimbi tena.

Wacha tupoteze wote
 
Serikali ya CCM haijawahi na haitawahi kumlazimisha msanii kuunga mkono itikadi zake. Huwa ni hiari yao wenyewe kuunga mkono itikadi ya CCM. WASANII WAKO HURU KUCHAGUA UPANDE WA KISIASA WANAOTAKA. NI HAKI YAO YA KIKATIBA.
 
Mkuu, waache hao wapuuzi

Wangekua wanafanya show, wanapiga pesa hafu wanakaa kimya tungejua ni wachakarikaji.

Tatizo linaanza wanaanza maneno ya kejeri na dharau mitandaoni.

Yaani wamevuka mipaka. Kusema kweli kwa upande wangu kuwasamehe ngumu sana

View attachment 3514526
Nimefuta nyimbo zao za recently zote nimebakisha old bongo fleva ambao 99% hawaimbi tena.

Wacha tupoteze wote
Wewe ni mtu mwenye roho mbaya
 
Wasanii wapambane kivyao thus it's necessary to be an entrepreneur instead of a businessman so that they could escape from that issue
 
Ila kusema kweli vijana wamepoteza radha sana, tena sana nafeel Iyo kitu

Itachukua mda mpaka mambo yawe sawa gharama ya damu ni kubwa sana

Ili warudi kwenye levo zao Inapaswa watume gharama iliyotozwa kwa ndugu zao nao ile kwao.!

Tupo tunasubiri masihi wa wasanii atakayekubali kukongomekwa kwa gharama ya wote
 
Fally Ipupa Nsimba anaimba vizuri sana, Ferre Gola répandre anaimba vizuri, nimechelewa sana kulijua jambo hili
 
Serikali ya CCM haijawahi na haitawahi kumlazimisha msanii kuunga mkono itikadi zake. Huwa ni hiari yao wenyewe kuunga mkono itikadi ya CCM. WASANII WAKO HURU KUCHAGUA UPANDE WA KISIASA WANAOTAKA. NI HAKI YAO YA KIKATIBA.
Sasa kwa nini manalialia wakiomba msamaha? Unaombaje msamaha bila kufanya kosa?
 
Fally Ipupa Nsimba anaimba vizuri sana, Ferre Gola répandre anaimba vizuri, nimechelewa sana kulijua jambo hili
King Kikii, Mpongo love, Monique seka, Tshala Muana, Mbilia Bel n.k wanamjua sana muziki.
 
Wakuu kabla ya kuwahukumu hawa viumbe tujikumbushe kuwa wasanii ni watu wenye ushawishi mkubwa kwenye jamii kuliko hata wanasiasa walio wengi. Kwa mfano Diamond peke yake ana ushawishi mkubwa kuliko wanasiasa wote wa nchi hii... kidunia hakuna Rais, mfalme au mtawala yeyote aliyekuwa akimzidi ushawishi hayati Michael Jackson kipindi akiwa hai.

Tawala karibu zote zinajua hilo ndo maana huwa zinawaweka karibu wasanii kwa kuwashawishi au kuwalazimisha kwa sababu kwa ushawishi walio nao ni hatari kuwaacha tu. Wakihamia kambi pinzani ni hatari kubwa. Wasanii wengi wamewahi kujikuta matatizoni kwa kusimama na itikadi tofauti na serikali iliyoko madarakani.

Mfano mrahisi ni majirani DRC zamani wakiitwa Zaire chini ya Dikteta Mobutu. Wasanii walipitia magumu kila walipokuwa wakionyesha misimamo yao inayokinzana na serikali. Hayati Franco aliwahi kukimbia nchi. Koffi Olomide mwaka 97 kama sio 98 aliwahi simamishwa barabarani na kushushwa kisha kucharazwa viboko na askari kama mtoto mdogo. Werrason alishushwa jukwaani akiwa anatumbuiza na kushushiwa kipigo cha mbwa mwizi. Kimsingi ni hatari kwa msanii kuwa na itikadi tofauti na serikali iliyopo madarakani. Hapa Tanzania mifano ipo na mnaijua.

Ninawasihi watanzania wote tusamehe hawa vijana kwa sababu wasingeweza kuepuka kukinywea kikombe walichokinywea.
Sawa waendelee kuwaimbia hao wahuni wa kijani,ila sisi wananchi tunao tekwa,kuuwawa na kubambikiwa kesi za hovyo hatuwataki.
 
Serikali ya CCM haijawahi na haitawahi kumlazimisha msanii kuunga mkono itikadi zake. Huwa ni hiari yao wenyewe kuunga mkono itikadi ya CCM. WASANII WAKO HURU KUCHAGUA UPANDE WA KISIASA WANAOTAKA. NI HAKI YAO YA KIKATIBA.
Wema,mlimpima mkojo kisa alikua chadema,acheni upuuzi.

Roma mlimteka hadi kakimbia nchi,na wengine wengi tu mmewafanyia maten
 
Back
Top Bottom