Wasanii 2O wakatwa katika list ya wasanii wa kutumbuiza kwenye Fiesta Dar

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,502
9,282
Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, Alhamisi hii katika kipindi cha Clouds360, amesema amepunguza wasanii 20 katika list ya wasanii ambao walipanga kuwepo kwenye show ya tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Jumamosi hii katika viwanjwa Leaders Club.

Ruge alisema miongoni mwa wasanii hao walioondolewa kisa muda ni pamoja na Lulu Diva, Zaiid, pamoja na ChinBeez.

‘’Tulikaa kama kamati jana tunatumia nguvu kubwa mno kwenye suala la muda wakati tuna shoo kubwa iliyokamilika, kwahiyo tumeamua kuachana na suala la muda,tumeamua tukae kwenye muda tulioupanga sisi na kuhakikisha tuna ‘six hours’ za entertainment ambazo zimepangwa na kupangika,” alisema Ruge.

Aliongeza, “Kitakachokosekana ni wale wasanii zaidi ya 20, kama, Bright, Mimi Mars,Lulu Diva, Zaiidyao, ChinBeez,hao bahati mbaya ni lazima tuwaondoe kwa sababu ya ratiba kubana kutokana na muda, tungeweza kuwaingiza lakini hatuna muda’’


BONGO 5
 
Link hii hapa Audio: Wasanii 2O wakatwa katika list ya Fiesta Dar – Bongo5.com sheria zinazingatiwa Dar kwingine wanapeta ili vijana wafaidi burudani mpaka kucheee.
 
sasa si waende kule kwenye tamasha la bure au napo booking imejaa
 
hata hao walikuwa wengi, masaa sita wasanii zaidi ya 20 kila mtu anatumbuiza kwa muda gani? masaa sita ni sawa na dakika 360, msanii anapaswa kutumbuiza nyimbo ngapi ili kweli pesa anayopata awe ameitolea jasho? weka wachache wenye maana watu wafurahi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…